Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 7:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Lakini, mufalme wa Misri akawaita wenye hekima wake na wachawi. Wale wachawi wa Misri wakafanya vile vile kwa uchawi wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 7:11
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kulipokuwa asubui, yeye akiwa na wasiwasi sana, aliwaita wachawi wote wa Misri, na wenye hekima, akawaambia ndoto zake. Lakini hakuna hata mumoja aliyeweza kumutafsiria ndoto zile.


Kila mumoja akatupa fimbo yake chini, ikakuwa nyoka. Lakini fimbo ya Haruni ikameza fimbo zao.


Lakini wachawi wa Misri kwa kutumia uchawi wao wakafanya vivyo hivyo. Kwa hiyo moyo wa mufalme wa Misri ukabaki kuwa mugumu, naye hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Lakini siku hiyo sehemu ya Goseni watu wangu wanakoishi nitaikinga. Kule mainzi wale hawatakuwa. Kwa hiyo utatambua kwamba mimi Yawe ninatenda mambo katika inchi yako.


Lakini wachawi wa Misri kwa uchawi wao vilevile wakaleta vyura katika inchi ya Misri.


Vyura wataondoka kwako, na kwenye nyumba zenu, kwa wakubwa wako na kwa watu wako. Watabaki tu katika muto Nili.”


Basi, mufalme akaamuru waganga, walozi na wachawi wa Wakaldea waletwe kusudi wamufasirie ndoto yake. Wote wakakuja na kusimama mbele yake.


Danieli akamujibu mufalme: Hakuna wenye hekima, wachawi, waganga wala waaguzi wanaoweza kukujulisha fumbo hilo lako.


Ee Beltesaza, unayekuwa mukubwa wa waganga, ninafahamu kuwa roho ya miungu mitakatifu iko ndani yako, na kwamba hakuna fumbo linalokuwa gumu kwako. Hii ndiyo ndoto yangu; uniambie maana yake.


Katika ufalme wako kuna mutu ambaye roho ya miungu mitakatifu iko ndani yake. Wakati wa utawala wa baba yako, mutu huyu alionekana kuwa mwenye ujuzi, ufahamu na hekima kama ya miungu. Baba yako, mufalme Nebukadneza, alimufanya kuwa mukubwa wa waaguzi, wachawi, Wakaldea wenye hekima, na waganga,


Mufalme Belsasari akaamuru kwa sauti kwamba wachawi, Wakaldea wenye hekima na waaguzi waletwe. Walipoletwa, mufalme akawaambia wenye hekima hao wa Babeli: Yeyote atakayesoma maandiko haya na kunijulisha maana yake, atavalishwa nguo nzuri nyekundu za kifalme na mukufu wa zahabu katika shingo lake, na kupewa nafasi ya tatu katika ufalme.


kwa maana kutatokea watu wanaojiita kwa uongo ‘Kristo’ pamoja na manabii wa uongo, nao wataonyesha vitambulisho vikubwa na maajabu, hata ikiwezekana, wawadanganye hata watu waliochaguliwa na Mungu.


Ee ninyi Wagalatia! Ninyi wajinga! Ni nani aliyewaloga? Habari juu ya kutundikwa kwa Yesu Kristo juu ya musalaba ilielezwa waziwazi mbele ya macho yenu.


Basi, hatutakuwa tena kama watoto, tukipeperushwa na kuvutwa na mafundisho ya kila aina yanayoletwa na watu wanaodanganya wengine na kuwapotosha kwa mayele yao.


Mwovu atakuja na uwezo wa Shetani na kufanya miujiza ya kila namna, vitambulisho na maajabu ya uongo.


Watu wale wanapinga ukweli kama vile Yane na Yambure walivyopingana na Musa. Akili ya watu hao imepotoka, nayo imani yao imegeuka bure.


Lakini hawataendelea mbali sana, kwa sababu upumbafu wao utaonekana wazi mbele ya watu wote, sawa ilivyokuwa kwa Yane na Yambure.


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


Wafilistini waliwaita makuhani na waaguzi wao na kuwauliza: “Tufanye nini na Sanduku hili la Yawe? Mutuambie namna gani tunavyoweza kulirudisha kwa nafasi yake.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ