Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 6:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Nilimutokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo nikijulikana kama Mungu Mwenye Nguvu, ingawa sikuwajulisha jina langu, Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 6:3
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Wakati Abramu alipokuwa na umri wa miaka makumi tisa na tisa, Yawe akamutokea, akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Uwezo. Uendelee mbele yangu na kuwa mukamilifu.


Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”


Mungu Mwenye Nguvu akubariki upate wazao wengi na kuongezeka, kusudi ukuwe jamii kubwa ya watu.


Tena Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu Mwenye Nguvu. Ujaliwe wazao wengi na kuongezeka. Taifa na kundi la mataifa watatokea kwako na wafalme watatokea katika uzao wako.


Yakobo akamwambia Yosefu: “Mungu Mwenye Nguvu alinitokea nilipokuwa kule Luzu katika inchi ya Kanana, akanibariki.


Lakini watu wa haki wanafurahi Mungu anapokuja, wanashangilia na kuimba kwa furaha.


Wafezeheke na kuhangaika milele, waangamie kwa haya kabisa.


Yawe ni shujaa kwa vita; Yawe ndilo jina lake.


Musikilize na kutii maneno atakayosema, wala musimwasi. Hatawasamehe uasi wenu maana nimemutuma kwa jina langu.


Mungu akamujibu: “Mimi Ndimi Ninayekuwa. Uwaambie watu wa Israeli kwamba: Yule anayeitwa Ndimi Ninayekuwa amekutuma kwao.


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Yawe, Mufalme na Mukombozi wa Israeli, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mimi ni wa kwanza na wa mwisho; hakuna mungu mwingine isipokuwa mimi.


Kwa hiyo, Yawe anasema: Wakati huu nitawafundisha kusudi wapate kutambua waziwazi nguvu zangu na uwezo wangu, nao watajua kwamba jina langu ni Yawe.


Yawe aliyeiumba dunia, Yawe aliyeifanya na kuiimarisha dunia, yule ambaye jina lake ni Yawe, anasema hivi:


Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Nanyi, enyi watu wangu, mutatambua kwamba mimi ni Yawe nitakapofunua makaburi yenu na kuwafufua kutoka ndani ya makaburi yenu.


Nitawatia mishipa na nyama, nitawafunika ngozi na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mutaishi. Hapo mutajua kwamba mimi ni Yawe.


Yesu akawajibu: “Kweli, kweli ninawaambia: mbele Abrahamu hajazaliwa, mimi nilikuwa niko.”


Ni mimi Yoane ninayewaandikia ninyi makanisa saba munaokuwa katika jimbo la Azia. Ninawatakia neema na amani kutoka kwa Mungu anayekuwa, aliyekuwa na anayekuja, na kutoka kwa roho saba wanaokuwa mbele ya kiti chake cha kifalme,


Naomi akasema: “Musiniite tena Naomi muniite Mara, kwa maana Mungu Mwenye Nguvu ameyafanya maisha yangu yakuwe machungu sana.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ