Kutoka jangwa la Sini, Waisraeli wote pamoja wakasafiri hatua kwa hatua kama vile Yawe alivyoamuru. Watu wakapiga kambi kule Refidimu. Lakini kule hakukukuwa maji ya kunywa.
Uwaambie Waisraeli kwamba: Yawe, Mungu wa babu zenu, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutuma kwao. Hili ndilo jina langu milele, na hivi ndivyo nitakavyokumbukwa katika vizazi vyote.
Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.
Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.