Lakini hesabu ya matofali yanayotengenezwa kila siku ikuwe ileile, wala kusipunguke hata tofali moja, kwa sababu watu hawa ni wavivu ndio maana wanapiga kelele na kusema: ‘Utuache tuende kutoa sadaka kwa Mungu wetu.’
Azaria mwana wa Hosaya, Yohana mwana wa Karea na watu wote wenye kiburi, walimwambia Yeremia: Yawe, Mungu wetu, hakukutuma wewe utuambie tusiende Misri, tuishi huko.
Babu zenu hawakupata azabu kwa sababu ya kukataa maagizo yangu na amri nilizowapa kwa njia ya watumishi wangu manabii? Wakati huo, wao waligeuka na kusema kwamba: Yawe wa majeshi alikusudia kututendea kulingana na mienendo yetu na matendo yetu, na kweli ndivyo alivyotutendea.
Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza?