Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 5:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Lakini mufalme wa Misri akawajibu: “Enyi Musa na Haruni, kwa nini munajaribu kuwatoa watu kwa kazi yao? Murudie kwa kazi yenu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 5:4
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.


Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake.


Zaidi ya hayo, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wamelazimishwa kufanya kazi za kitumwa na Wamisri, nikalikumbuka agano langu.


Wakubwa wakamwambia mufalme: Inafaa mutu huyu auawe kwa maana anawavunja moyo waaskari ambao wameachwa katika muji huu na watu wote kwa jumla, kwa kusema maneno kama hayo. Yeye hawatakii watu hawa mema lakini mabaya.


Basi, Amazia kuhani wa muji wa Beteli, akamupelekea mufalme Yeroboamu wa Israeli habari hii: Amosi analeta fitina juu yako katika ufalme wa Israeli. Hotuba zake ni hatari kwa inchi hii.


Wakaanza kumushitaki, wakisema: “Tulimukuta mutu huyu akiwashawishi watu wa taifa letu kufanya uasi. Yeye alikuwa akiwaambia kwamba wasilipe kodi kwa Mufalme wa Roma. Na zaidi ya hii anasema kwamba yeye ndiye Kristo, Mufalme aliyengojewa.”


Tumetambua kwamba mutu huyu ni wa hatari sana, ameanzisha fujo kati ya Wayuda wote katika dunia. Tena yeye ni mukubwa wa chama cha Wanazareti.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ