Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 5:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Musa na Haruni wakamwambia: “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tunakusihi utuache tujiendee katika jangwa mwendo wa siku tatu tutoe sadaka kwa Yawe, Mungu wetu. Kama sivyo, yeye atatuua kwa ugonjwa mukali au kwa upanga.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 5:3
12 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi ikatokea kwamba walipoanza kukaa mule, hawakumwabudu Yawe, kwa hiyo Yawe akatuma simba kati yao, nao wakawaua wamoja kati yao.


Sasa musikuwe wenye mioyo migumu kama babu zenu lakini mumutii Yawe. Mukuje katika Pahali Patakatifu pake Yerusalema, ambako ametakasa milele, mumwabudu Yawe, Mungu wenu, kusudi asiwakasirikie.


Kila kitu Mungu wa mbinguni alichoagiza kwa ajili ya nyumba yake, kinapaswa kutimizwa kikamilifu, kusudi asipate kukasirikia ufalme wangu au wana wangu.


“Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mutamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: ‘Yawe, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu katika jangwa, tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka.’


Kisha umwambie hivi: Yawe, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, naye anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waende zao kusudi wanitumikie katika jangwa. Lakini mpaka sasa wewe haupendi kutii.


Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni anyooshe mukono wake na kuinua fimbo yake juu ya mito, juu ya mifereji na visima, nao vyura watatokea na kuenea kila pahali katika inchi ya Misri.”


Yawe akafanya kama vile alivyosema. Makundi makubwa ya mainzi yakashambulia nyumba ya mufalme wa Misri, nyumba za wakubwa wake na inchi nzima ya Misri. Inchi nzima ya Misri ikaharibiwa na mainzi wale.


Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Wale mainzi wakatoweka kutoka kwa mufalme wa Misri, wakubwa wake na watu wake, wala hakukubaki hata mumoja.


Bwana wetu Yawe akaniambia hivi: Upige mikono, piga kishindo kwa muguu na kusema: Ole kwenu Waisraeli kwa sababu ya machukizo yenu yote; kwa sababu mutakufa kwa upanga, njaa na kwa ugonjwa mukali.


Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.


Atawaletea ugonjwa mukali mpaka ninyi wote muangamie kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ