Tangu wakati ule nilipowaongoza watu wa Israeli kutoka Misri mpaka hivi leo, sijaishi katika nyumba. Nimekuwa nikihama toka hema hata hema, na toka makao hata makao mengine.
Waisraeli watengeneze sanduku la mbao za mujohoro, lenye urefu wa sentimetre mia moja na kumi, upana sentimetre makumi sita na sita, na urefu kwenda juu sentimetre makumi sita na sita.
Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.
Utatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya samawi, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Juu ya pazia lile utachora kwa ufundi sanamu za makerubi.
Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na kunyunyiza kwa kidole chake upande wa mashariki juu ya kiti cha rehema kisha atainyunyizia mbele ya Sanduku la Agano mara saba kwa kidole chake.
Wakati wa kuvunja kambi, Haruni na wana wake wataingia katika hema, na kushusha pazia linalokuwa mbele ya Sanduku la Agano, kisha walifunike kwa pazia hilo.
Kisha hekalu la Mungu linalokuwa mbinguni likafunguliwa, na Sanduku la Agano lake likaonekana ndani yake. Halafu kukatokea umeme, makelele, ngurumo ya radi, tetemeko la inchi na mvua kubwa ya mawe.