Tangu wakati ule nilipowaongoza watu wa Israeli kutoka Misri mpaka hivi leo, sijaishi katika nyumba. Nimekuwa nikihama toka hema hata hema, na toka makao hata makao mengine.
Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.
Hiyo itakuwa ndani ya hema la mukutano inje ya pazia lile mbele ya Sanduku la Agano na Haruni na wana wake wataitunza mbele yangu tangu magaribi mpaka asubui. Sharti hili lifuatwe siku zote na Waisraeli wote, kizazi kwa kizazi.
Kisha utasagwa na kufanya unga laini, upate kutumiwa ndani ya hema la mukutano na kulipakaa Sanduku la Agano, pahali nitakapokutana nawe. Huo utakuwa ubani mutakatifu kabisa kwenu.
Katika mwaka wa makumi mbili na tano tangu tulipopelekwa katika uhamisho, siku ya kumi ya mwezi wa kwanza, siku hiyo Yawe alinijaza uwezo wake. Ilikuwa mwaka wa kumi na ine tangu pale Yerusalema ulipotekwa.
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:
Siku Musa alipomaliza kusimamisha hema takatifu, akalimiminia mafuta na kulitakasa pamoja na vyombo vyake vyote. Akamiminia mazabahu mafuta na kuitakasa pamoja na vyombo vyake vyote.
Siku ambayo hema takatifu lilisimikwa, wingu likashuka na kufunika hema la kuchunga vibao vya agano. Wakati wa usiku wingu hilo lilionekana kama moto mpaka asubui.