Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 4:23 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

23 Nami ninakuambia: Umwache mwana wangu aondoke, kusudi anitumikie! Kama ukikataa kumwachilia aondoke, angalia nitamwua muzaliwa wako wa kwanza mwanaume.’ ”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 4:23
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Aliua wazaliwa wa kwanza katika inchi yao, ndilo chipukizi la kwanza la jamaa za Wamisri.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, wazaliwa wa watu na wa nyama vilevile.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza wa Misri. Wema wake unadumu milele.


Aliwaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri; ndilo chipukizi la kwanza katika kambi la Hamu.


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Ukikataa kuwaacha watu wangu waondoke, basi, kesho nitaleta nzige washambulie inchi yako.


Nitakapopita, kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri atakufa, kuanzia muzaliwa wa kwanza wako wewe mufalme wa Misri ambaye ni murizi wako, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mujakazi anayesaga ngano kwa jiwe. Hata wazaliwa wa kwanza wa mifugo nao wote watakufa.


Katikati ya usiku, Yawe akawaua wazaliwa wa kwanza wote wa Misri. Wote walikufa, tangu muzaliwa wa kwanza wa mufalme wa Misri, murizi wa ufalme, mpaka muzaliwa wa kwanza wa mufungwa katika kifungo. Hata wazaliwa wa kwanza wa nyama nao walikufa.


Mufalme wa Misri kwa ugumu wake alikataa kutuachilia tuondoke. Kwa hiyo Yawe akamwua kila muzaliwa wa kwanza katika inchi ya Misri, muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu na wa nyama. Basi, mimi ninamutolea Yawe sadaka kila muzaliwa wa kwanza dume wa mifugo yangu. Lakini kila muzaliwa wa kwanza wa wana wangu ninamukomboa.’


Musa akamwelezea baba mukwe wake mambo yote Yawe aliyomutendea mufalme wa Misri na Wamisri kwa ajili ya Waisraeli. Akamwambia vilevile juu ya shida zote zilizowapata katika safari na jinsi Yawe alivyowaokoa.


“Wao watakusikiliza, nawe pamoja na wazee wa Waisraeli mutamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: ‘Yawe, Mungu wa Waebrania, ametutokea. Sasa, uturuhusu tuende safari ya mwendo wa siku tatu katika jangwa, tumutolee Yawe, Mungu wetu, sadaka.’


Kisha, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri, wakamwambia: “Yawe, Mungu wa Israeli anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke, wanifanyie sikukuu katika jangwa.’ ”


“Kwenda kwa mufalme wa Misri, umwambie awaache Waisraeli waondoke katika inchi yake.”


Kisha umwambie hivi: Yawe, Mungu wa Waebrania, amenituma kwako, naye anasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waende zao kusudi wanitumikie katika jangwa. Lakini mpaka sasa wewe haupendi kutii.


Yawe akamwambia Musa: “Umwambie Haruni anyooshe mukono wake na kuinua fimbo yake juu ya mito, juu ya mifereji na visima, nao vyura watatokea na kuenea kila pahali katika inchi ya Misri.”


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Kesho amuka asubui mapema umwendee mufalme wa Misri wakati anapokwenda kwenye muto umwambie: ‘Yawe anasema hivi: Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Kama ukikataa kuwaacha waondoke, basi, nitakuletea makundi ya mainzi, wewe, wakubwa wako na watu wako wote. Wataingia kwenye nyumba zenu na nyumba zote za Wamisri zitajaa makundi ya mainzi na inchi yote ya Misri vilevile.


Yawe akafanya kama vile alivyosema. Makundi makubwa ya mainzi yakashambulia nyumba ya mufalme wa Misri, nyumba za wakubwa wake na inchi nzima ya Misri. Inchi nzima ya Misri ikaharibiwa na mainzi wale.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Kwenda kwa mufalme wa Misri umwambie kwamba mimi Yawe, Mungu wa Waebrania, ninasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Kisha, Yawe akamwambia Musa: “Kesho, amuka asubui mapema umwendee mufalme wa Misri, umwambie kwamba mimi Yawe, Mungu wa Waebrania, ninasema hivi: ‘Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Kama ukikataa kuwaacha waondoke na ukiendelea kuwashikilia,


Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ