Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 4:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Yawe akamwambia Musa: “Unashika nini katika mukono wako?” Musa akamwambia: “Fimbo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 4:2
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yakobo akatwaa fito mbichi za miti ya mulubna, lozi na mwaramoni, akazimenya maganda mistari nyeupe ionekane katika fito hizo.


Elisha akamwuliza: “Sasa nikusaidie namna gani? Uniambie kile unachokuwa nacho kwako.” Mama yule mujane akamujibu: “Mimi mutumishi wako sina kitu chochote lakini chupa ndogo ya mafuta.”


Yawe ataeneza mamlaka yako kutoka Sayuni; utatawala juu ya waadui zako wote.


Utatwaa katika mukono wako fimbo hii ambayo utaitumia kufanya vile vitambulisho.”


Basi, Musa akatwaa muke wake na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Katika mukono wake alishika ile fimbo aliyoamuriwa na Mungu aitwae.


Basi, kwenda ukutane naye kesho asubui, wakati anapokwenda kwenye muto Nili. Umungojee kando ya muto. Utwae katika mukono wako ile fimbo iliyogeuka kuwa nyoka.


“Mufalme wa Misri atakapowaambia muhakikishe jambo lile kwa kutenda miujiza, wewe utamwambia Haruni atwae fimbo yake, aitupe mbele ya mufalme, nayo itakuwa nyoka.”


Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.


Kuelekea mifugo, kila nyama wa kumi ni mutakatifu kwa Yawe.


Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ