Elisha akamwuliza: “Sasa nikusaidie namna gani? Uniambie kile unachokuwa nacho kwako.” Mama yule mujane akamujibu: “Mimi mutumishi wako sina kitu chochote lakini chupa ndogo ya mafuta.”
Basi, Musa akatwaa muke wake na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Katika mukono wake alishika ile fimbo aliyoamuriwa na Mungu aitwae.
Basi, kwenda ukutane naye kesho asubui, wakati anapokwenda kwenye muto Nili. Umungojee kando ya muto. Utwae katika mukono wako ile fimbo iliyogeuka kuwa nyoka.
Ee Mungu, uwachunge watu wako kwa fimbo yako, uwachunge wale wanaokuwa kundi lako mwenyewe ambao wanaishi peke yao katika pori na kuzungukwa na inchi yenye mboleo. Uwachunge kama ulivyofanya pale zamani katika shamba la malisho ya Basani na Gileadi.