Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 4:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Musa akarudi kwa Yetro, baba mukwe wake, akamwambia: “Tafazali uniruhusu nirudie Misri kwa wandugu zangu, nione kama wangali wazima.” Yetro akamwambia: “Kwenda kwa amani.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 4:18
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi ni Yosefu. Baba yangu angali muzima?” Lakini wandugu zake wakapigwa na bumbuazi mbele yake, hata wakashindwa kumujibu.


Elisha akamutuma mutumishi wake amwambie: “Kwenda uoge mara saba katika muto Yordani, nawe utapona kabisa.”


Elisha akamwambia: “Kwenda kwa amani.” Namani akaenda zake. Alipokuwa bado hajafika mbali,


Musa akakubali kukaa kwa yule mutu. Basi, yule mutu akamupa Musa binti yake anayeitwa Zipora akuwe muke wake.


Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.


Lakini Yesu akamwambia tena yule mwanamuke: “Kwenda na amani, imani yako imekuokoa.”


Nyuma ya siku chache, Paulo akamwambia Barnaba: “Turudi sasa kwa kuwaangalia wandugu waamini katika miji ambamo tulihubiri neno la Bwana, kusudi tuone kama wako katika hali gani.”


Yule mulinzi wa kifungo akamwelezea Paulo habari ile akimwambia: “Wakubwa wametuma habari kwamba mufunguliwe. Basi sasa mutoke na kujiendea na amani.”


Watu wote wanaokuwa watumwa wanapaswa kuwaheshimu wabwana wao kabisa, kusudi watu wasitukane jina la Mungu na kuzarau mafundisho yetu.


Yule kuhani akawaambia: “Muende kwa amani. Yawe anaichunga safari yenu.”


Halafu Eli akamwambia: “Kwenda kwa amani; naye Mungu wa Israeli akupe kile ulichomwomba.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ