Yawe, Mungu wa mbingu, aliyenitoa katika nyumba ya baba yangu na kutoka katika inchi nilimozaliwa, na ambaye alisema nami, aliniapia kwamba atawapa wazao wangu inchi hii. Yeye atamutuma malaika wake mbele yako kusudi umuletee mwana wangu muke kutoka kule.
Uwaagize wasimamizi wale wakusanye chakula chote katika miaka saba inayokuja ya mavuno kwa wingi. Ngano hiyo iwekwe chini ya mamlaka yako, ee mufalme, ikuwe akiba ya chakula kwa miji yote, nao waitunze ngano hiyo.
na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”
naye akatembea mwendo wa siku nzima kuingia katika jangwa. Basi, akafika, akaikaa chini ya muti mumoja wa muretemu. Halafu, akaomba apate kufa, akisema: “Inatosha! Siwezi tena. Ee Yawe, sasa utoe uzima wangu. Mimi si bora kuliko babu zangu.”
Halafu hasira ya Mungu ikawaka juu ya Musa, akamwambia: “Si kuna ndugu yako Haruni ambaye ni Mulawi? Ninajua yeye anajua kusema vizuri. Tena anakuja kukutana nawe, na mara tu atakapokuona atafurahi ndani ya moyo.
Lakini ninaposema “Sitamutaja tena Yawe, wala sitasema tena kwa jina lake”, ndani yangu kunawaka kitu kama moto uliofungiwa ndani ya mifupa yangu. Ninajaribu sana kuuzuia humo, lakini ninashindwa.
Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.
Kapiteni wa mashua akamwendea, akamwambia: Namna gani wewe unaweza kulala? Amuka umwombe Mungu wako; labda Mungu wako atatuhurumia na kuyaokoa maisha yetu.
Mwana wa Mutu atawatuma wamalaika wake, nao watakusanya toka katika Ufalme wake watu wote wanaowaangusha wengine katika zambi pamoja na wote wanaofanya maovu.
Malaika wa Yawe aliondoka Gilgali, akaenda Bokimu, akawaambia Waisraeli: “Niliwaondoa katika inchi ya Misri na kuwaleta katika inchi ambayo niliahidi kwa kiapo kwa babu zenu. Nilisema kwamba sitalivunja agano langu nanyi hata kidogo.