Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Basi, kwenda! Mimi nitaongoza kinywa chako na kukufundisha cha kusema.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 4:12
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.


Unifundishe kutimiza mapenzi yako, maana wewe ni Mungu wangu! Roho wako muzuri aniongoze katika njia sawa.


Usikuwe mupumbafu kama farasi au nyumbu, ambao lazima wafungwe kamba ndani ya kinywa, kama sivyo hawatakukaribia.”


Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”


Lakini Musa akasema: “Ee Bwana wangu, tafazali ninakusihi, umutume mutu mwingine.”


Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidia na kuwafundisha mambo mutakayofanya.


Haruni ataongea na Waisraeli kwa ajili yako. Yeye atakuwa musemaji wako, nawe utakuwa kama Mungu kwake.


Alifanya maneno yangu kuwa makali kama upanga mukali, alinificha katika kivuli cha mukono wake; aliufanya ujumbe wangu kuwa mukali kama chongo ya mushale, akanificha kama mushale ndani ya mufuko wake.


Bwana wetu Yawe amenifundisha jinsi ya kusema, kusudi niwatie moyo wale waliochoka. Kila asubui ananipa hamu ya kusikiliza mambo anayotaka kunifundisha.


Kisha Yawe akanyoosha mukono wake, akagusa kinywa changu, akaniambia: Nimetia maneno yangu ndani ya kinywa chako.


Hapo Musa akawaambia watu: Hivi ndivyo mutakavyotambua kwamba Yawe ndiye aliyenituma kufanya mambo haya yote, wala siyo kwa mapenzi yangu mwenyewe.


Na mutakapokamatwa na kupelekwa kwa kuhukumiwa, musijihangaishe mbele ya wakati juu ya maneno mutakayosema, lakini museme maneno mutakayopewa saa ile ile. Kwa sababu hayatatoka kwenu wenyewe, lakini yatatoka kwa Roho Mutakatifu.


Ilikuwa siku moja, Yesu alikuwa nafasi fulani akiomba. Alipomaliza kuomba, mumoja kati ya wanafunzi wake akamwambia: “Bwana, utufundishe kuomba, kama vile Yoane alivyowafundisha wanafunzi wake.”


Lakini Musaidizi, ndiye Roho Mutakatifu, yule Baba atakayemutuma kwa jina langu, atawafundisha maneno yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.


Muniombee vilevile, kusudi Mungu anijalie maneno ya kusema. Kwa hiyo nitaweza kuwajulisha watu kwa uhodari siri ya Habari Njema.


Nitawachagulia kati ya wandugu zao wenyewe nabii kama wewe, nitatia maneno yangu ndani ya kinywa chake, naye atawaambia yote nitakayomwamuru.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ