Zile incha mbili za mukufu wa zahabu utazishikamanisha kwenye zile kingo mbili za kile kifuko kusudi zishikamane na kipande cha mabega cha kizibao upande wa mbele.
Wakafua zahabu na kuikata katika nyuzi nyembamba kwa kuzifuma pamoja na sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa kwa ufundi.
Mukaba uliofumwa kwa ufundi juu yake kwa kuifunga ulikuwa kitu kimoja na kizibao hicho, na ulitengenezwa kwa vitu hivyohivyo: zahabu, sufu ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, kama vile Yawe alivyomwamuru Musa.