Kutoka 38:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
9 Kisha akatengenezea hema upango. Mapazia ya upande wa kusini wa upango yalikuwa ya kitani safi iliyosokotwa na yenye urefu wa metre makumi ine na ine;
Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.
nayo yalishikiliwa na nguzo makumi mbili za shaba zenye vikalio makumi mbili vya shaba. Lakini vifungio vya nguzo hizo na kamba zake vilikuwa vya feza.
mapazia ya upango unaokuwa kati ya hema takatifu na mazabahu, na pazia la mulango wa upango, na kamba zake. Kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa zao.
mapazia na kamba za upango unaokuwa kandokando ya hema na mazabahu, mapazia ya mulango wa kiwanja, na vifaa vyote vinavyotumika pamoja na vitu hivi. Wao watashugulika na mambo yote yanayoelekea vitu hivi.