Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 38:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha akatengenezea hema upango. Mapazia ya upande wa kusini wa upango yalikuwa ya kitani safi iliyosokotwa na yenye urefu wa metre makumi ine na ine;

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 38:9
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alijenga uwanja wa ndani ambao kuta zake zilikuwa za mistari tatu ya mawe yaliyochongwa, na mustari moja wa boriti za mwerezi.


Muingie ndani ya hekalu lake kwa shukrani, muingie katika kiwanja chake kwa kumusifu. Mumushukuru na kulisifu jina lake.


Ee Mungu, umwangalie huyo ngao yetu, upendezwe na huyo uliyemuchagua.


Ee Yawe wa majeshi, kweli makao yako yanapendeza!


Nani katika mbingu anayeweza kulinganishwa nawe, ee Yawe? Nani anayekuwa sawa nawe kati ya miungu?


Watu wa haki wanastawi kama mingazi; wanakomaa kama mierezi ya Lebanoni!


Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.


nayo yalishikiliwa na nguzo makumi mbili za shaba zenye vikalio makumi mbili vya shaba. Lakini vifungio vya nguzo hizo na kamba zake vilikuwa vya feza.


Kwa mwisho Musa akatengeneza upango kuzunguka hema takatifu na mazabahu na kuweka pazia kwenye mulango wa upango. Hivyo, Musa akakamilisha kazi yote.


Utazungusha upango na kutundika pazia kwenye mulango wake.


mapazia ya upango unaokuwa kati ya hema takatifu na mazabahu, na pazia la mulango wa upango, na kamba zake. Kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa zao.


mapazia na kamba za upango unaokuwa kandokando ya hema na mazabahu, mapazia ya mulango wa kiwanja, na vifaa vyote vinavyotumika pamoja na vitu hivi. Wao watashugulika na mambo yote yanayoelekea vitu hivi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ