Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 38:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha akatengeneza birika la shaba na tako lake la shaba. Birika hilo lilitengenezwa kwa kutumia vioo vya shaba vya wanawake waliotumika kwenye mulango wa hema la mukutano.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 38:8
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hiramu alitengeneza vilevile mabeseni kumi ya shaba, moja kwa kila gari. Kila beseni ilikuwa na upana wa metre moja na sentimetre makumi ine na tano, na iliweza kujaa maji kadiri ya litre elfu moja na mia sita.


Kisha, akatengeneza birika la maji la muviringo, lenye upana wa metre ine na nusu kutoka ukingo mpaka ukingo, lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na lenye muzunguko wa metre kumi na tatu na nusu.


Ninanawa mikono yangu kuonyesha kama sina kosa, na kuizunguka mazabahu yako, ee Yawe,


mazabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika la maji pamoja na tako lake,


Akaitia ile miti katika zile pete zilizokuwa kando ya mazabahu kwa kuibebea. Mazabahu hiyo iliyotengenezwa kwa mbao ilikuwa wazi ndani.


Birika la kunawia utaliweka katikati ya hema la mukutano na mazabahu na kulijaza maji.


Heri mutu anayenisikiliza, anayeikaa kila siku kwenye mulango wangu, anayekesha karibu na milango yangu.


nguo nzuri, shemizi nzuri, vioo na vitambaa mbalimbali.


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Wakati ule Petro alikuwa akiikaa inje katika kiwanja. Mutumishi mumoja mwanamuke akamufikia na kumwambia: “Wewe vilevile ulikuwa pamoja na Yesu wa Galilaya.”


Kisha akabaki mujane, hata akaeneza umri wa miaka makumi nane na mine. Alibaki katika hekalu, akitumikia Mungu usiku na muchana, akifunga kula chakula na kuomba.


Yesu akamwambia: “Aliyekwisha kuoga hahitaji kunawa tena, isipokuwa miguu yake tu, kwa maana mwili wake wote ni safi. Na ninyi ni safi, lakini si wote.”


Lakini Petro alisimama inje karibu na mulango. Yule mwanafunzi mwingine, aliyejulikana na Kuhani Mukubwa, akatoka inje, akasema na mwanamuke aliyelinda mulango, naye akamwachilia Petro kuingia ndani.


Mujane wa kweli asiyekuwa na mutu yeyote wa kumusaidia, anamutumainia Mungu, na kudumu kumutolea mahitaji yake na kumwomba muchana na usiku.


Hizo ni kanuni za kimutu zinazoelekea vyakula na vinywaji pamoja na desturi mbalimbali za utakaso za kidini. Nazo zinaamuriwa kushikwa mpaka upate kutimia wakati wa kutengeneza vitu vyote upya.


Watoto wangu, mutu asiwadanganye! Mutu anayetenda mambo ya haki ni mwenye haki kama vile Kristo ni mwenye haki.


na kutoka kwa Yesu Kristo. Yeye ni mushuhuda mwaminifu, naye ndiye wa kwanza aliyefufuliwa, vilevile yeye ni mukubwa wa wafalme wa dunia. Yeye anatupenda na ametukomboa toka katika zambi zetu kwa njia ya damu yake.


Wakati ule, Eli alikuwa muzee sana. Aliposikia yote ambayo wana wake walikuwa wanawatendea Waisraeli, jinsi walivyokuwa wanalala na wanawake waliokuwa wanatumika kwenye mulango wa Hema ya Kusanyiko,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ