Lakini sasa, ee Yawe, Mungu wetu, kwa muda mufupi umetuonyesha huruma yako na kuwawezesha wamoja kati yetu kuponyoka kutoka katika utumwa na kuishi kwa usalama pahali pako patakatifu. Pahali pa utumwa, umetupa furaha na maisha mapya.
Hii ndiyo hesabu ya vifaa vilivyotumika katika kujenga hema la kuchunga vile vibao vya agano. Hesabu hii ilitayarishwa na Walawi kwa amri ya Musa, chini ya uongozi wa Itamari mwana wa kuhani Haruni.
Muangalie Sayuni tunamofanyia sikukuu zetu; muangalie Yerusalema, makao matulivu, hema imara; misumari yake haitaongolewa hata kidogo, kamba zake hazitakatwa hata moja.
Mutu yule hashikamani na Kristo anayekuwa kichwa cha mwili. Chini ya uongozi wa Kristo, mwili muzima unakulishwa vizuri na kuunganishwa pamoja kwa njia ya maunganio na vifundo vyake, kusudi upate kukomaa kufuatana na mapenzi ya Mungu.