Akatengeneza mazabahu kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto. Mazabahu hiyo ilikuwa ya muraba, metre mbili na sentimetre makumi mbili kwa metre mbili na sentimetre makumi mbili, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili.
Akatengeneza vilevile vyombo vyote kwa ajili ya mazabahu: vyungu, majembe, mabeseni, kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote akavitengeneza kwa shaba.