Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 38:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Pazia la mulango wa upango lilitengenezwa kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kupambwa vizuri. Nalo lilikuwa na urefu wa metre tisa na urefu kwenda juu metre mbili, kulingana na mapazia ya upango.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 38:18
5 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akatengeneza pazia kwa kitambaa cha kitani safi, cha rangi ya samawi, ya rangi nyekundu-nyeusi na nyekundu. Akalichora kwa michoro ya makerubi.


Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.


Kwa ajili ya mulango wa hema utatengeneza pazia zito kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kuchorwa vizuri.


Vikalio vyote vya nguzo vilikuwa vya shaba, lakini vifungio vya nguzo hizo na kamba zake vilikuwa vya feza. Vifungio vyake vilikuwa vya feza; vilevile nguzo zake zote zilishikamanishwa kwa fito za feza.


Vilevile nguzo zake zilikuwa ine na vikalio vine vya shaba. Vifungio vyake vilikuwa vya feza, hata nguzo zake na kamba zake vilikuwa vya feza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ