Mimi nitakutana nawe pale. Kutoka juu ya kiti kile cha rehema katikati ya makerubi wale wanaokuwa juu ya Sanduku la Agano, nitazungumuza nawe na kukupa amri zote kwa ajili ya Waisraeli.
Yawe alipomaliza kuongea na Musa juu ya mulima Sinai, akamupatia Musa vile vibao viwili vya mawe ambavyo juu yake Mungu aliziandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.
Hivi ndivyo Yawe alivyokuwa akiongea na Musa uso kwa uso, kama mutu na rafiki yake. Kisha Musa alirudi tena katika kambi. Naye kijana Yoshua mwana wa Nuni ambaye alikuwa mutumishi wake hakuondoka ndani ya hema.
Kila mara Musa alipotoka kwenda kwenye hema hilo, kila mutu alisimama kwenye mulango wa hema yake na kumwangalia Musa mpaka alipoingia ndani ya hilo hema.
Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.
Nitashuka kule na kuzungumuza nawe; nitatwaa sehemu ya roho niliyokupa, niwape watu hao. Nao watabeba muzigo wa kuwatunza watu hawa pamoja nawe, kusudi usibebe muzigo huo peke yako.
Wakati Musa alipoingia ndani ya hema la mukutano kwa kuongea na Yawe, akasikia sauti kutoka upande wa juu wa kiti cha rehema, kilichokuwa juu ya Sanduku la Agano, kutoka kati ya wale makerubi.
Yawe akamwambia Musa: “Siku yako ya kuaga dunia imekaribia. Umwite Yoshua, mukuje pamoja katika hema la mukutano kusudi nimupe maagizo.” Basi, Musa na Yoshua wakaenda katika hema la mukutano,