Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 32:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ninawafahamu watu hawa. Wao wana vichwa vigumu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 32:9
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wao hawakutii; walikuwa wagumu kama babu zao ambao hawakumwamini Yawe, Mungu wao.


Sasa musikuwe wenye mioyo migumu kama babu zenu lakini mumutii Yawe. Mukuje katika Pahali Patakatifu pake Yerusalema, ambako ametakasa milele, mumwabudu Yawe, Mungu wenu, kusudi asiwakasirikie.


Lakini wao na babu zetu wakakuwa na kiburi na wakakuwa wagumu wakakataa kufuata maagizo yako.


Wakakataa kutii; hawakukumbuka maajabu uliyofanya kati yao. Wakakuwa wagumu, wakajichagulia kiongozi wa kuwarudisha katika utumwa katika inchi ya Misri. Lakini wewe Mungu uko mwepesi kwa kusamehe, mwenye huruma na rehema, haukasiriki upesi, uko mwema sana. Haukuwatupilia


wasikuwe kama vile babu zao walivyokuwa, watu wagumu na waasi, kizazi ambacho hakikuwa na musimamo kamili, ambacho hakikuwa na uaminifu kwa Mungu.


Muende katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali. Lakini kwa sababu ninyi ni wenye vichwa vigumu sitakwenda pamoja nanyi, nisiwaangamize katika njia.


Walifanya hivyo maana Yawe alikuwa amemwambia Musa: Uwaambie Waisraeli: Ninyi ni watu wenye vichwa vigumu. Nikienda pamoja nanyi kwa muda mufupi tu, nitawaangamiza. Hivyo muvue mapambo yenu kusudi nijue namna ya kuwatendea.


Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Lakini nilikujua wewe kuwa na moyo mugumu; kichwa kigumu kama chuma, uso wako kama shaba.


Nimeyaona machukizo yako: nimeona uzinzi wako na utongozaji wako, na uasherati wako usiousikilia haya, unaoufanya juu ya milima na katika mashamba. Ole kwako wewe Yerusalema! Mpaka wakati gani utabaki bila kutakaswa?


Nimeona jambo la kuchukiza sana kati ya Waisraeli: watu wa Efuraimu wanakimbilia miungu mingine, Waisraeli wamejichafua.


Kisha Yawe akamwambia Musa: Watu hawa watanizarau mpaka wakati gani? Na mpaka wakati gani wataendelea kutoniamini, hata pamoja na vitambulisho vyote nilivyotenda kati yao?


“Ninyi watu wagumu! Ninyi wenye roho ya kipagani na masikio yanayofungana! Siku zote munapingana na Roho Mutakatifu sawa vile babu zenu walivyofanya!


Kwa hiyo, mutahiri magovi ya mioyo yenu, musikuwe wagumu tena.


Maana ninajua jinsi munavyokuwa waasi na wagumu. Ikiwa mumemwasi Yawe wakati niko muzima pamoja nanyi, itakuwa namna gani nyuma ya kifo changu?


“Vilevile, Yawe akaniambia: ‘Nimewaona watu hawa, ni watu wagumu sana.


Basi, mujue kwamba Yawe, Mungu wenu, anawapa inchi hii nzuri muirizi si kwa sababu munastahili kuirizi, maana ninyi ni watu wagumu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ