Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 32:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kisha Haruni akamujengea yule mwana-ngombe mazabahu, halafu akatangaza: Kesho kutakuwa sikukuu kwa ajili ya Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 32:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Barua zenyewe ziliandikwa hivi: “Mutangaze kwa watu kwa kufanya sikukuu ya kufunga kula, mukutane na kumupa Naboti nafasi ya heshima kati ya watu.


Yehu akaamuru: “Mutangaze mukutano wa ibada ya Bali!” Tangazo likatolewa,


Uria akajenga mazabahu ile kulingana na mufano ule na kuimaliza mbele ya kurudi kwa Ahazi.


Kwa hiyo wakaamua kutoa tangazo katika inchi yote ya Israeli, kutoka Beri-Seba mpaka Dani, kwamba watu wakuje Yerusalema kwa kufanya sikukuu ya Pasaka ya Yawe, Mungu wa Israeli. Ilikuwa imepita muda murefu mbele ya watu kufanya Pasaka kulingana na sheria zake.


Musa akamujibu: “Kila mutu, vijana na wazee, tutaondoka na watoto wetu wanaume na wanawake, kondoo na mbuzi wetu na ngombe. Kwa maana tunapaswa kumufanyia Yawe sikukuu.”


Vizazi hata vizazi mutakumbuka tukio hilo kwa sikukuu kubwa kwa heshima yangu mimi Yawe. Hilo litakuwa agizo la milele kwenu.”


Musa akajenga mazabahu na kuita mazabahu hiyo “Yawe ni Bendera Yangu”,


Naye akazitwaa akaziyeyusha, akatengeneza sanamu ya mwana-ngombe. Watu wakapaaza sauti wakasema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri.


Kesho yake watu wakaamuka mapema wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Watu wakaikaa chini kwa kula na kunywa, kisha wakasimama na kucheza.


Watu wa Efuraimu wamejijengea mazabahu nyingi, na mazabahu hizo zimewazidishia zambi.


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Uwaambie Waisraeli hivi: Katika sikukuu zangu mimi Yawe ambazo zimepangwa mutakuwa na mukutano mutakatifu. Sikukuu ambazo nimepanga ni hizi:


Siku hiyohiyo mutatoa tangazo ya mukutano mutakatifu. Musifanye kazi. Hili ni sharti la kufuata milele katika vizazi vyenu vyote, katika makao yenu.


Hizo ndizo sikukuu za Yawe zilizopangwa ambazo mutatoa tangazo kuwe mukutano mutakatifu wa kumutolea Yawe sadaka zinazotolewa kwa moto, sadaka za kuteketezwa na sadaka za vyakula, matoleo na sadaka za kinywaji, kila moja kwa siku yake yenyewe.


Sikukuu zingine zangu mimi Yawe ambazo mutakuwa na mukutano mutakatifu zitafanyika katika wakati huu uliopangwa.


Kwa hiyo tufanye karamu yetu ya Pasaka pasipo kutumia mikate iliyotiwa chachu; ni kusema pasipo zambi na uovu. Lakini tutumie mikate isiyotiwa chachu; ni kusema katika usafi na ukweli.


Saulo akamujengea Yawe mazabahu. Hiyo ilikuwa ndiyo mazabahu ya kwanza ambayo Saulo alimujengea Yawe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ