Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 3:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 na hivyo, nimeshuka kusudi niwaokoe toka mikono ya Wamisri. Nitawatoa katika inchi na kuwapeleka katika inchi nzuri na kubwa, inchi inayotiririka maziwa na asali, inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 3:8
54 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akashuka chini kuona muji ule na munara ambayo wanadamu walijenga.


Basi, tushuke chini na kuvuruga luga yao kusudi wasielewane wao kwa wao.”


Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.


Hata hivyo, nitaazibu taifa watakalotumikia na kwa mwisho watatoka wakiwa na mali nyingi.


Hivyo nitashuka kwenda kule nijionee mwenyewe kama kweli wamefanya kadiri ya kilio kilichonifikia. Ninataka kujua.”


Hapo Israeli, baba yao, akawaambia: “Basi! Kwa vile ni lazima ikuwe hivyo basi, mufanye hivi: mutwae katika mifuko yenu sehemu ya mazao bora ya inchi yetu, mumupelekee zawadi yule mukubwa. Mumupelekee mafuta kidogo ya mukwaju, asali kidogo, ubani, marasi, kungu na lozi.


Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe kule Misri na kukurudisha huku. Utakapokufa, mukono wa Yosefu ndio utakaofumba macho yako.”


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


Ukamwona kuwa wa haki mbele yako; ukafanya agano naye kuwapa wazao wake inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi na Wagirgasi. Na ahadi yako ukaitimiza; maana wewe ni mwaminifu.


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Lakini Yawe anasema: “Kwa sababu wamasikini wanaugua, na wakosefu wanalia, sasa ninasimama, nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”


Malaika wa Yawe anawalinda wote wanaomwabudu, na kuwaokoa kutoka katika hatari.


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.


Siku hiyohiyo Yawe aliwatoa Waisraeli katika inchi ya Misri kwa makundi.


Na wakati Yawe atakapowafikisha katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Wahivi, na Wayebusi, inchi ambayo aliwaapia babu zenu kwamba atawapa ninyi, inchi inayotiririka maziwa na asali, munapaswa kushika sikukuu hii kila mwaka katika mwezi huu wa kwanza.


Ninaahidi kwamba nitawatoa katika mateso yenu kule Misri na kuwapeleka katika inchi ya Wakanana, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. Nitawapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali.’


Mushike amri ninazowapa leo. Nitawafukuza mbele yenu Waamori, Wakanana, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Tangu nilipokwenda na kuongea na mufalme wa Misri kwa jina lako, yeye amewatendea watu hawa uovu. Wewe haujafanya lolote kwa kuwakomboa watu wako.”


mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika inchi kama hii yenu, inchi yenye ngano na divai, inchi yenye mukate na mashamba ya mizabibu.


Ingeteketea kama moto unavyochoma kichaka, kama vile moto unavyochemusha maji. Ukuje upate kuwajulisha waadui zako jina lako nayo mataifa yatetemeke mbele yako!


Na kwa njia hiyo mimi nitatimiza ahadi niliyowatolea babu zenu, kwamba nitawapa inchi inayojaa maziwa na asali, kama inavyokuwa hata leo. Nami nikajibu: Ikuwe hivyo, ee Yawe.


Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.


Uliwapa inchi hii ambayo uliahidi kuwapa babu zao, inchi inayotiririka maziwa na asali.


Siku hiyo niliwaapia kwamba nitawatoa katika inchi ya Misri na kuwapeleka mpaka kwenye inchi niliyowachagulia, inchi ya maziwa na asali na inchi nzuri kuliko inchi zote.


Lakini, nimekwisha kuwaambia: Mutarizi inchi yao, mimi ninawapa inchi hiyo ikuwe yenu, inchi inayotiririka maziwa na asali. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatenga na mataifa mengine.


Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


mupeleleze jinsi inchi inavyokuwa. Muchunguze vilevile kama watu wanaoishi mule ni wenye nguvu au wazaifu, wengi au wachache.


Mupeleleze kama inchi hiyo ni nzuri au mbaya, na kama miji wanamoishi ni kambi au ni nyumba zilizozungukwa na kuta.


Wakamwambia Musa: Tuliifikia inchi uliyotutuma tuipeleleze; hiyo ni inchi inayotiririka maziwa na asali, na hili ni tunda lake.


Na zaidi ya hii hakuna mutu aliyepanda mbinguni, isipokuwa Mwana wa Mutu aliyeshuka toka mbinguni.


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Waliporudi, wakatuletea matunda mamoja ya inchi hiyo na wakatuarifu kwamba inchi hiyo Yawe, Mungu wetu, anayotupatia ni nzuri.


Sasa muvunje kambi yenu muendelee na safari. Muende kwenye inchi ya milima ya Waamori na maeneo ya inchi jirani katika Araba, kwenye milima na mabonde, huko Negebu na sehemu za pembeni ya bahari. Muende mpaka inchi ya Kanana, na inchi ya Lebanoni, mpaka kwenye ule muto mukubwa Furati.


Juu yake mutaandika maneno yote ya sheria hizi zote, mutakapoingia katika inchi ile inayotiririka maziwa na asali, ambayo Yawe, Mungu wa wazee wenu, aliwaahidi.


Yawe atawafanikisha kwa wingi: watoto, mifugo na mavuno katika shamba katika inchi aliyowaapia wazee wenu kwamba atawapa.


Kwa hiyo enyi Waisraeli, mukuwe waangalifu kwa kuzitimiza, kusudi mufanikiwe na kuongezeka sana katika inchi hiyo inayotiririka maziwa na asali kama vile alivyowaahidi.


“Yawe, Mungu wenu atawafikisha kwenye inchi ambayo mutakwenda kufanya makao yenu na atafukuza mataifa mengi kutoka inchi hiyo. Mutakapoingia, atafukuza mbele yenu mataifa saba makubwa na yenye nguvu kuliko ninyi: Wahiti, Wagirgasi, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi.


Waisraeli walisafiri kwa muda wa miaka makumi ine katika jangwa hata wanaume wote waliokuwa na umri wa kwenda kwa vita wakaangamia kwa kuwa hawakusikiliza mambo Yawe aliyosema. Yawe alikuwa amewaapia watu hao kwamba hawataiona inchi ile inayotiririka maziwa na asali ambayo yeye aliwaapia baba zao kwamba atawapa.


Wafalme wote waliokuwa ngambo ya muto Yordani katika inchi ya milima na kwenye mabonde na eneo lote la pembeni ya bahari ya Mediteranea kuelekea Lebanoni, Wahiti, Waamori, Wakanana, Waperizi, Wahivi na Wayebusi waliposikia habari za Waisraeli,


Lakini Waisraeli wakawajibu hao Wahivi: “Tunaweza namna gani kufanya agano nanyi? Labda ninyi munaishi karibu nasi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ