Kutoka 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
7 Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,
Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.
Naye akaniambia: ‘Angalia mabeberu wote wanaowapanda madike wana mistari, madoadoa na matakamataka. Jambo hili limekuwa hivyo kwa sababu nimeona jinsi Labani alivyokutendea.
Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”
“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.
Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.
Sasa basi, ninakusihi, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, unionyeshe sasa njia zako, kusudi nipate kukujua na kupata kukubaliwa mbele yako. Ninaomba ukumbuke vilevile kwamba taifa hili ni watu wako.
Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.
Hakika nimeona namna watu wangu Waisraeli wanavyoteswa katika inchi ya Misri. Nimesikia kilio chao nami nimeshuka kwa kuwaokoa. Sasa kuja, nitakutuma kule Misri.’
Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.
“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”