Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Kisha Yawe akamwambia: “Nimeona mateso ya watu wangu wanaokuwa katika inchi ya Misri na nimesikia kilio chao kinachosababishwa na watesaji wao. Ninajua mateso yao,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 3:7
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha huyo malaika wa Yawe akamwambia: “Wewe una mimba na utazaa mutoto mwanaume; utamwita Isimaeli, maana Yawe ameyaona mateso yako.


Hivyo nitashuka kwenda kule nijionee mwenyewe kama kweli wamefanya kadiri ya kilio kilichonifikia. Ninataka kujua.”


Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.


Lea akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume, akamwita Rubeni, akisema: “Yawe ameona mateso yangu; bila shaka sasa mume wangu atanipenda.”


Naye akaniambia: ‘Angalia mabeberu wote wanaowapanda madike wana mistari, madoadoa na matakamataka. Jambo hili limekuwa hivyo kwa sababu nimeona jinsi Labani alivyokutendea.


Kama Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu ambaye ni kitisho cha Isaka, asingelikuwa upande wangu, hakika ungeliniacha niondoke mikono mitupu. Lakini Mungu aliona mateso yangu na kazi niliyofanya kwa mikono yangu, akakukaripia usiku wa kuamukia leo.”


Wewe unawaokoa wanyenyekevu, lakini unaangalia wenye majivuno kusudi uwashushe.


Yoahazi akamusihi Yawe, naye Yawe alipoona jinsi mufalme wa Aramu alivyowatesa watu wa Israeli akasikia maombi yake.


“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.


Uliyaona mateso ya babu zetu walipokuwa katika inchi ya Misri, na walipokuomba musaada kwenye bahari Nyekundu ukawasikiliza.


Hata hivyo Mungu aliona taabu yao, wakati aliposikia kilio chao;


Lakini Yawe anasema: “Kwa sababu wamasikini wanaugua, na wakosefu wanalia, sasa ninasimama, nami nitawapa usalama wanaoutazamia.”


Ninamutolea malalamiko yangu, ninamwelezea taabu zangu.


Anajibia mahitaji yao wote wanaomwabudu; anasikia kilio chao na kuwaokoa.


“Enyi munaomwabudu Yawe, mumusifu! Mumutukuze, enyi wazao wote wa Yakobo! Mumwogope Mungu, enyi wazao wote wa Israeli!


Mumutukuze Yawe pamoja nami, wote pamoja tulisifu jina lake.


Mumugeukie Mungu mupate kufurahi; nanyi hamutafezeheka hata kidogo.


Lakini wewe Yawe unaona jambo hilo. Usinyamaze, ee Yawe, usikae mbali nami.


Ee Yawe, wewe unayeniopoa kutoka nguvu za kifo, uangalie mateso wale wanaonichukia wanayoniletea na kunirehemu


Basi, Wamisri wakachagua wakubwa wawasimamie Waisraeli na kuwatesa kwa kazi ngumu. Waisraeli wakafanya kazi ya kumujengea mufalme wa Misri miji ya kuwekea akiba, Pitomu na Ramesesi.


Basi, kukatokea mufalme mwingine kule Misri ambaye hakumujua Yosefu.


na hasira yangu itawaka, nami nitawaua ninyi kwa upanga, na wake zenu watakuwa wajane na watoto wenu wayatima.


Sasa basi, ninakusihi, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, unionyeshe sasa njia zako, kusudi nipate kukujua na kupata kukubaliwa mbele yako. Ninaomba ukumbuke vilevile kwamba taifa hili ni watu wako.


Basi, wakubwa na wasimamizi wa watu wakatoka na kuwaambia watu: “Mufalme wa Misri anasema hivi: ‘Sitawapa nyasi.


Siku hiyohiyo mufalme wa Misri aliwaamuru wakubwa pamoja na wasimamizi, akasema:


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Tukamulilia Yawe, naye akasikia kilio chetu, akatuletea malaika aliyetuondoa Misri. Sasa tuko hapa Kadesi, muji unaopakana na inchi yako.


Hakika nimeona namna watu wangu Waisraeli wanavyoteswa katika inchi ya Misri. Nimesikia kilio chao nami nimeshuka kwa kuwaokoa. Sasa kuja, nitakutuma kule Misri.’


Kwa maana tuko na Kuhani Mukubwa asiyekosa kujua mwenyewe uzaifu wetu. Maana yeye alijaribiwa katika njia zote sawasawa na sisi, lakini hakufanya zambi.


“Kesho, wakati kama huu, nitakuletea mutu kutoka inchi ya kabila la Benjamina, nawe utamupakaa mafuta kuwa mutawala wa watu wangu Waisraeli. Yeye atawaokoa watu wangu kutoka kwa Wafilistini, maana nimeyaona mateso ya watu wangu na kilio chao kimenifikia.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ