Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yawe alipoona kwamba Musa amegeuka kwa kuangalia kichaka, akamwita pale kutoka kichaka: “Musa! Musa!” Musa akaitika: “Niko hapa. Ninasikiliza!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 3:4
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo yale, Mungu alimupima Abrahamu. Mungu alimwita: “Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa.”


Lakini malaika wa Yawe akamwita kutoka mbinguni: “Abrahamu! Abrahamu!” Naye akaitika: “Niko hapa!”


Kisha Yakobo akaamuka toka usingizi, akasema: “Hakika, Yawe yuko pahali hapa, nami sikujua!”


Mungu akaongea na Israeli katika maono usiku, akamwita: “Yakobo! Yakobo!” Yakobo akaitika: “Niko hapa.”


Musitegemee kutesa, musijisifie mali ya wizi; kama mali zikiongezeka, musizitegemee.


Basi, Musa akapanda juu kwenye mulima kwa Mungu. Halafu Yawe akamwita Musa kutoka kule juu ya mulima, akamwambia: “Hivi ndivyo utakavyowaambia wazao wa Yakobo, wale Waisraeli:


Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.


Musa akamwambia Yawe: Wewe unaniambia: Uwaongoze watu hawa, lakini haujanijulisha ni nani utakayemutuma anisaidie. Hata hivyo umesema kwamba unanijua kwa jina langu na vilevile kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako.


Yawe akamwambia: “Hivyo Waisraeli watapata kuamini kwamba mimi Yawe, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, nimekutokea.”


Yawe akamwita Musa na kuongea naye katika hema la mukutano, akamwambia:


Kisha akasikia sauti ikimwambia: “Petro, simama. Chinja na ukule!”


Siku moja, ilipokuwa saa tisa ya muchana, akaona maono. Aliona waziwazi malaika wa Mungu akiingia kwake na kumwambia: “Kornelio!”


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Inchi yake ijae yote yanayokuwa mazuri, ibarikiwe kwa huruma wa Yawe, ambaye alitokea katika kichaka. Baraka hizi zishukie watu wa kabila la Yosefu, aliyekuwa mukubwa kati ya wandugu zake.


Kisha Yawe akakuja na kusimama hapo, akamwita Samweli kama pale mbele: “Samweli! Samweli!” Samweli akasema: “Sema, maana mimi mutumishi wako ninasikiliza.”


Halafu Yawe akamwita Samweli, naye Samweli, akaitika: “Niko hapa!”


Yawe akamwita tena: “Samweli!” Samweli akaamuka, akamwendea Eli na kumwambia: “Nimekuja, maana umeniita.” Lakini Eli akamwambia: “Sikukuita mwana wangu, ulale tena.”


Yawe akamwita Samweli kwa mara ya tatu. Samweli akaamuka, akamwendea Eli na kumwambia: “Nimekuja, maana umeniita.” Halafu Eli alitambua kwamba Yawe ndiye aliyemwita Samweli.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ