Kutoka 3:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.
Mungu akamusikia mutoto yule akilia, na malaika wa Mungu akamwita Hagari kutoka mbinguni, akamwambia: “Una shida gani Hagari? Usiogope. Mungu amesikia sauti ya mutoto kule anapokuwa.
na malaika ambaye aliniokoa katika mabaya yote, awabariki vijana hawa! Jina langu na majina ya babu zangu, Abrahamu na Isaka, yadumishwe katika vijana hawa; nao waongezeke kwa wingi katika dunia.”
Mulima wa Sinai ulikuwa umefunikwa na moshi kwa sababu Yawe alishuka juu yake katika moto. Moshi wa moto ule ulipanda juu kama moshi wa furu kubwa na mulima wote ukatetemeka kwa nguvu.
Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!
Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.
Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.
Maliwali, wasimamizi, wakubwa wa majimbo na washauri wa mufalme, wote wakakusanyika pamoja, wakaona kwamba ule moto haukuweza kuwaunguza hao watatu. Nywele zao hazikuungua, nguo zao hazikuungua wala hawakuwa na harufu yoyote ya moto.
Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.
Na juu ya kufufuka kwa wafu, hamujasoma katika kitabu cha Sheria ya Musa, yale maandiko yanayosema juu ya kichaka kilichowaka moto? Mungu alimwambia Musa: ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’ ”
Musa alionyesha waziwazi kwamba wafu watafufuka. Katika maandiko yake yanayosema juu ya kichaka kilichowaka moto, yeye anamutaja Bwana kuwa ni ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka na Mungu wa Yakobo.’
Mungu alitimiza mambo yale Sheria ya Musa iliyoshindwa kuyatimiza, kwa sababu ya ukosefu wa nguvu unaotokana na hali zaifu ya kimwili. Mungu alitoa hukumu juu ya zambi inayotawala mwili kwa kutuma mwana wake wa peke katika hali ya kimutu, mwenye hali zaifu ya zambi kwa ajili ya kuondoa zambi.
Inchi yake ijae yote yanayokuwa mazuri, ibarikiwe kwa huruma wa Yawe, ambaye alitokea katika kichaka. Baraka hizi zishukie watu wa kabila la Yosefu, aliyekuwa mukubwa kati ya wandugu zake.
na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,