Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 3:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kwenda uwakusanye wazee wa Israeli na kuwaambia kwamba: Yawe, Mungu wa babu wao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, amekutokea na kusema: ‘Nimewachunguza ninyi na kuyaona mambo munayotendewa katika inchi ya Misri!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 3:16
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ikakuwa hivyo. Mungu akafanya anga, akatenga maji yanayokuwa juu ya anga na yale yanayokuwa chini ya anga lile.


Yawe akamukumbuka Sara, akamutendea kama alivyoahidi.


Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.


Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,


Kisha Yosefu akawaambia wandugu zake: “Mimi sasa ninakaribia kufa. Lakini Mungu hakika atawafikia kwa kuwasaidia. Atawatoa katika inchi hii na kuwapeleka katika inchi aliyowaapia Abrahamu, Isaka na Yakobo.”


akasikia malalamiko ya wafungwa, akawaachilia huru waliohukumiwa kuuawa.


Yawe anawaangalia wale wanaomwabudu, watu ambao wanatumainia wema wake.


Nikiangalia mbingu uliyoumba kwa vidole vyako, mwezi na nyota ulizozisimika huko,


Basi, kukatokea mufalme mwingine kule Misri ambaye hakumujua Yosefu.


Musa alipeleka mifupa ya Yosefu kama vile Yosefu alivyoagiza mbele ya kufa kwake. Alikuwa amewaapisha Waisraeli akisema: “Mungu atakapowafikia kuwatoa katika inchi hii, munapaswa kupeleka mifupa yangu kutoka hapa pamoja nanyi.”


Watu wa mataifa wamesikia hayo wakatetemeka; Wafilistini wamepatwa na kitisho.


Yawe akamwambia Musa: “Pita mbele ya watu hawa ukipeleka wazee wao wamoja. Twaa vilevile katika mukono wako ile fimbo uliyoipiga nayo muto Nili.


Halafu Yetro, baba mukwe wa Musa, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine. Naye Haruni akakuja pamoja na wazee wa Israeli kwa kula chakula pamoja na Yetro, mbele ya Yawe.


Mungu akawaangalia Waisraeli, naye akatambua hali yao.


Na Mungu hakuwazuru wale viongozi wa watu wa Israeli. Walimwona Mungu, wakakula na kunywa.


Basi, malaika wa Yawe akamutokea katika mwali wa moto katikati ya kichaka. Musa akaangalia, akashangaa kuona kichaka kinawaka moto na wala hakiungui.


Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.


Musa akamwambia Mungu: “Lakini Waisraeli hawataniamini wala kunisikiliza. Watasema kwamba wewe Yawe haukunitokea.”


Kisha Musa na Haruni wakaenda, wakawakusanya wazee wote wa Waisraeli.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Yawe akamwambia: “Hivyo Waisraeli watapata kuamini kwamba mimi Yawe, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, nimekutokea.”


Wakubwa wa makuhani na wasimamizi wa watu wakakusanyika ndani ya nyumba ya Kuhani Mukubwa, aliyeitwa Kayafa,


“Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


Nao wakafanya vile, wakatuma misaada waliyokusanya kwa wazee wa kanisa kwa mukono wa Barnaba na Saulo.


Simoni anatoka kutuelezea namna Mungu alivyowashugulikia watu wa mataifa mengine pale mbele kusudi ajichagulie wamoja kati yao kuwa watu wake wa pekee.


Toka Mileto, akatuma ujumbe Efeso kwa kuwaita wazee wa kanisa.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Kisha, Naomi akapata habari kwamba Yawe alikuwa amewabariki watu wake kwa kuwapa chakula. Basi, akaondoka kutoka Moabu kurudi kwao, pamoja na wakwe zake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ