Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 3:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 3:12
43 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyuma ya mambo hayo, neno la Yawe lilimufikia Abramu katika maono kusema hivi: “Abramu! Usiogope! Mimi ni ngao yako. Zawadi yako itakuwa kubwa!”


Lakini Abramu akamwambia: “Ee Yawe, nitajua namna gani kwamba nitarizi inchi hii?”


Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.


Kisha Yawe akamwambia Yakobo: “Rudia katika inchi ya wazee wako na kwa jamaa yako, nami nitakuwa pamoja nawe.”


“Na hiki ndicho kitakuwa kitambulisho kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka unaokuja mutakula kinachoota chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mutapanda na kuvuna mavuno; mutapanda mizabibu na kula matunda yake.


Finehasi mwana wa Eleazari, alikuwa musimamizi wao, zamani, Yawe alikuwa pamoja naye.


Unionyeshe kitambulisho cha wema wako, ee Yawe, kusudi wale wanaonichukia wafezeheke, wanapoona umenisaidia na kunifariji.


Yetro, baba mukwe wa Musa, alikuja pamoja na binti yake, ni kusema muke wa Musa, pamoja na watoto. Akamukuta Musa katika jangwa alikokuwa amepiga kambi kwenye mulima wa Mungu.


Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.


Halafu, Musa akamwambia Mungu: “Sasa, nikiwaendea Waisraeli na kuwaambia: ‘Mungu wa babu zenu amenituma kwenu’, nao wakiniuliza: ‘Jina lake ni nani?’, nitawaambia nini?”


Mungu akasema: Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe na nitakupa raha.


Basi, kwenda! Mimi nitaongoza kinywa chako na kukufundisha cha kusema.”


Wewe utaongea naye na kumwambia yote atakayosema. Mimi nitawasaidia na kuwafundisha mambo mutakayofanya.


Yawe akafanya kama vile Musa alivyomwomba. Wale mainzi wakatoweka kutoka kwa mufalme wa Misri, wakubwa wake na watu wake, wala hakukubaki hata mumoja.


Na hiki ndicho kitakuwa kitambulisho kwako Hezekia: Mwaka huu na mwaka unaokuja mutakula kinachoota chenyewe bila kupandwa. Lakini katika mwaka wa tatu mutapanda na kuvuna mavuno; mutapanda mizabibu na kula matunda yake.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Basi, Bwana mwenyewe atawapa kitambulisho: bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume na kumwita jina lake “Emanueli – Mungu Yuko Pamoja Nasi”.


Wewe usiwaogope watu hao. Niko pamoja nawe kwa kukulinda. –Ni ujumbe wa Yawe.


Hapo Musa akawaambia watu: Hivi ndivyo mutakavyotambua kwamba Yawe ndiye aliyenituma kufanya mambo haya yote, wala siyo kwa mapenzi yangu mwenyewe.


Yawe hajaona ubaya kwa watu wa Yakobo, wala uovu kwa hao watu wa Israeli. Yawe Mungu wao yuko pamoja nao, Yeye anasifiwa kwa vigelegele kati yao, yeye anapokea sifa zao za kifalme.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Nao wanafunzi wakaenda kuhubiri fasi zote. Bwana akatumika pamoja nao na kuhakikisha ukweli wa mahubiri yao kwa njia ya vitambulisho walivyofanya.]


Na Bwana akawaongoza kwa uwezo wake, hata watu wengi sana wakaamini neno la Bwana na kumugeukia.


Lakini mimi nitaazibu taifa lile litakalowafanya kuwa watumwa. Kisha nitawaondoa katika inchi ile, nao wataniabudu kwenye nafasi hii.’


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


Kisha Yawe akamwagiza Yoshua, mwana wa Nuni, akamwambia: “Ukuwe imara na hodari, maana utawaongoza Waisraeli katika inchi ambayo nimewaapia kuwapa, nami nitakuwa pamoja nawe.”


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Hakuna mutu atakayekushinda siku zote za maisha yako. Nitakuwa pamoja nawe kama nilivyokuwa pamoja na Musa. Siku zote nitakuwa nawe wala sitakuacha hata kidogo.


Malaika wa Yawe akamutokea, akamwambia: “Yawe yuko pamoja nawe, ewe shujaa.”


Yawe akamwambia: “Nitakuwa pamoja nawe; nawe utawaangamiza Wamidiani sawa vile wangekuwa mutu mumoja.”


Gideoni akamwambia: “Basi, ikiwa nimepata rehema kwako, unionyeshe kitambulisho kusudi nijue kwamba ni wewe kweli uliyezungumuza nami.


Malaika wa Yawe akanyoosha fimbo yake, akagusa nyama na mikate kwa incha ya fimbo. Kwa rafla, moto ukatoka ndani ya jiwe, ukateketeza nyama na mikate. Mara moja malaika wa Yawe akatoweka mbele yake.


Kule utasikia wanayosema, nawe utapata nguvu za kuweza kwenda kuwashambulia.” Basi, Gideoni akaenda pamoja na mutumishi wake Pura mpaka kwenye vituo vya walinda zamu wa kambi ya Wamidiani.


Lakini wakisema sisi tuwaendee, basi tutawaendea maana hicho kitakuwa ni kitambulisho kwamba Yawe amewatia katika mikono yetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ