Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Sasa, nitakutuma kwa mufalme wa Misri kusudi uwatoe watu wangu, watu wale wa Israeli, kutoka katika inchi ya Misri.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 3:10
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia Abramu: “Ujue hakika kwamba wazao wako watakaa kama wageni katika inchi isiyokuwa yao, watakuwa watumwa na watateswa kwa muda wa miaka mia ine.


Hata hivyo, nitaazibu taifa watakalotumikia na kwa mwisho watatoka wakiwa na mali nyingi.


Kisha akamutuma Musa mutumishi wake, akamutuma pamoja na Haruni muchaguliwa wake.


Wewe ukajifanyia njia juu ya bahari; ulitembea juu ya maji yale mengi, lakini pahali ulipopita hapakuonekana.


Waisraeli walikuwa wameishi katika inchi ya Misri kwa muda wa miaka mia ine na makumi tatu.


Katika siku ya mwisho ya mwaka wa mia ine na makumi tatu, siku ileile ndipo makabila yote ya Yawe yaliondoka katika inchi ya Misri.


Musa akamwambia Yawe: Wewe unaniambia: Uwaongoze watu hawa, lakini haujanijulisha ni nani utakayemutuma anisaidie. Hata hivyo umesema kwamba unanijua kwa jina langu na vilevile kwamba nimepata kukubaliwa mbele yako.


Sasa basi, ninakusihi, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, unionyeshe sasa njia zako, kusudi nipate kukujua na kupata kukubaliwa mbele yako. Ninaomba ukumbuke vilevile kwamba taifa hili ni watu wako.


Haruni na Musa ndio walioambiwa na Yawe: “Mutoe watu wa Israeli kutoka inchi ya Misri, vikundi kwa vikundi.”


Yakobo alikimbilia katika inchi ya Aramu. Akiwa huko alifanya kazi kusudi apate mwanamuke, akachunga kondoo kusudi apate mwanamuke.


Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.


Hakika nimeona namna watu wangu Waisraeli wanavyoteswa katika inchi ya Misri. Nimesikia kilio chao nami nimeshuka kwa kuwaokoa. Sasa kuja, nitakutuma kule Misri.’


Yeye ndiye aliyewaongoza Waisraeli toka Misri akifanya maajabu na vitambulisho katika inchi ile, na kwenye bahari Nyekundu na katika jangwa kwa muda wa miaka makumi ine.


Mungu alimwambia: ‘Wazao wako wataishi katika inchi ya kigeni, na kule watafanywa kuwa watumwa, nao watateswa kwa muda wa miaka mia ine.


Lakini mimi nitaazibu taifa lile litakalowafanya kuwa watumwa. Kisha nitawaondoa katika inchi ile, nao wataniabudu kwenye nafasi hii.’


Yawe akamugeukia, akamwambia: “Kwenda kwa uwezo unaokuwa nao, uikomboe Israeli kutoka Wamidiani. Ni mimi ninayekutuma.”


Samweli akawaambia: “Yawe ndiye aliyemuchagua Musa na Haruni na kuwaondoa babu zenu katika inchi ya Misri.


“Yakobo na jamaa yake walipokwenda Misri, na Wamisri walipowagandamiza, babu zenu walimulilia Yawe. Naye akawatuma Musa na Haruni ambao waliwatoa babu zenu katika inchi ya Misri na kuwafanya mukae katika inchi hii.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ