Hiramu alitengeneza vilevile vyungu, kanya na mabakuli. Basi, Hiramu akamaliza kazi aliyoamuriwa na mufalme Solomono juu ya nyumba ya Yawe: nguzo mbili, mabakuli mawili ya taji zilizowekwa juu ya nguzo, nyavu mbili kwa ajili ya kufunika hizo taji mbili, mifano ya makomamanga mia ine kwa ajili ya nyavu hizo mbili, mistari miwili ya makomamanga kwa kila wavu kwa kupamba zile taji mbili zilizokuwa juu ya nguzo, magari kumi, vikingio kumi katika magari hayo, birika lile moja, sanamu za ngombe dume kumi na wawili, chini ya hilo birika, la vyungu vya kuwekea majivu, majembe, na mabeseni. Vitu hivi vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe ambavyo Hiramu alimutengenezea mufalme Solomono, vilikuwa vya shaba iliyoangarishwa.