Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 27:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Utaitengenezea vyombo vyake: vyungu vya kuwekea majivu, majembe, na mabeseni, na kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote utavitengeneza kwa shaba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 27:3
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hiramu alitengeneza vilevile vyungu, kanya na mabakuli. Basi, Hiramu akamaliza kazi aliyoamuriwa na mufalme Solomono juu ya nyumba ya Yawe: nguzo mbili, mabakuli mawili ya taji zilizowekwa juu ya nguzo, nyavu mbili kwa ajili ya kufunika hizo taji mbili, mifano ya makomamanga mia ine kwa ajili ya nyavu hizo mbili, mistari miwili ya makomamanga kwa kila wavu kwa kupamba zile taji mbili zilizokuwa juu ya nguzo, magari kumi, vikingio kumi katika magari hayo, birika lile moja, sanamu za ngombe dume kumi na wawili, chini ya hilo birika, la vyungu vya kuwekea majivu, majembe, na mabeseni. Vitu hivi vyote vilivyokuwa katika nyumba ya Yawe ambavyo Hiramu alimutengenezea mufalme Solomono, vilikuwa vya shaba iliyoangarishwa.


Vilevile walipeleka vyungu, majembe, makasi na miiko iliyotumiwa kwa kuchoma ubani na vyombo vingine vyote vya shaba nyeusi vilivyotumiwa katika kazi ya hekalu,


wakapeleka vyetezo na mabakuli. Mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme akapeleka mbali kila chombo cha zahabu na kila chombo cha feza.


vilevile alitoa maagizo juu ya kiasi cha zahabu safi iliyohitajika kwa kutengeneza makanya, mabeseni na vikombe, vilevile kiasi cha zahabu na feza iliyohitajika kwa kutengeneza mabakuli ya zahabu na ya feza,


Hiramu akatengeneza vyungu, vipao na mabeseni. Basi Hiramu akamaliza kazi aliyomufanyia mufalme Solomono juu ya nyumba ya Mungu;


Halafu vyungu, vipao na kanya na vyombo vingine vyote vya nyumba ya Yawe ambavyo Huruma-Abi alimutengenezea mufalme Solomono, vilikuwa vya shaba iliyoangarishwa.


Musa akachota nusu ya damu ya nyama wale na kuiweka katika mabeseni na nusu ingine akainyunyiza juu ya mazabahu ile.


Vyombo vyote vya hema takatifu vya matumizi ya kila aina, pamoja na misumari vyote na hata vile vya kiwanja, vitakuwa vya shaba.


Katika kila pembe ya mazabahu ile utatengeneza upembe ambao utakuwa umeundwa kutokana na mazabahu yenyewe. Mazabahu ile yote utaipakaa shaba.


Kisha utatengeneza wavu wa shaba wenye pete ine za shaba kwenye pembe zake ine.


Akatengeneza vilevile vyombo vyote kwa ajili ya mazabahu: vyungu, majembe, mabeseni, kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote akavitengeneza kwa shaba.


Halafu atatwaa chetezo na kutwaa makaa toka kwenye mazabahu mbele ya Yawe na mikono miwili ya ubani uliosagwa vizuri sana na atauleta ndani ya pazia.


Juu yake wataweka vyombo vyote vinavyotumika katika ibada kwenye mazabahu: vyetezo, makanya, miiko na mabakuli. Kisha, juu yake watatandaza kifuniko cha ngozi laini ya mbuzi na kuiingiza miti yake ya kulibebea.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ