Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 27:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Katika kila pembe ya mazabahu ile utatengeneza upembe ambao utakuwa umeundwa kutokana na mazabahu yenyewe. Mazabahu ile yote utaipakaa shaba.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 27:2
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Naye Adonia, kwa sababu alimwogopa Solomono, akakimbilia katika hema la Yawe, akazishika pembe za mazabahu apate kuponyoka.


Yoabu alipopata habari, alikimbilia katika hema ya Mungu na kushikilia pembe za mazabahu kwa maana alikuwa amemwunga Adonia mukono ingawa mbele hakukuwa na Abusaloma.


Siku hiyohiyo, mufalme aliizindua sehemu ya katikati ya uwanja uliokuwa mbele ya nyumba ya Yawe, maana ni pale ndipo alipotolea sadaka za kuteketezwa, sadaka za ngano, na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu ile mazabahu ya shaba haikutosha kwa sadaka hizo zote.


Mazabahu ya shaba ambayo ilitakaswa kwa ajili ya Yawe, aliiondoa mbele ya nyumba kutoka nafasi yake katikati ya mazabahu yake na nyumba ya Yawe, akaiweka kwenye nafasi iliyokuwa upande wa kaskazini wa mazabahu yake.


Mufalme Solomono alitengeneza birika la maji la muviringo lenye urefu wa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano na upana sawa na metre kenda, na urefu wake kwenda juu metre ine na nusu.


Yawe ni Mungu; yeye ametujalia mwangaza wake. Mushike matawi katika mikono, mukiandamana mpaka kwenye mazabahu.


Utaitengenezea vyombo vyake: vyungu vya kuwekea majivu, majembe, na mabeseni, na kanya na visahani vya kutwalia moto. Vyombo vyake vyote utavitengeneza kwa shaba.


Utatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu kwa kidole chako, na damu yote inayobaki utaimwanga chini ya mazabahu.


Bezaleli akatumia shaba hiyo kwa kutengeneza vikalio vya mulango wa hema la mukutano, mazabahu ya shaba pamoja na wavu wake wa shaba, vyombo vyote vya mazabahu,


Sehemu hii ya juu, ambayo itatumika kuteketezea sadaka, itakuwa muraba, kila upande metre mbili. Mujengo wa pembe za sehemu hii ya juu zitainuka kuliko sehemu zingine.


Kisha atatoka na kwenda kwenye mazabahu inayokuwa mbele ya Yawe na kufanya ibada ya upatanisho. Atatwaa sehemu ya damu ya yule ngombe dume na ya yule mbuzi na kupakaa pembe za mazabahu pande zote.


Kisha, sehemu ya damu atazipakaa kwenye pembe za mazabahu inayokuwa katika hema la mukutano mbele ya Yawe. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Kuhani atachovya kidole chake katika damu ya sadaka kwa ajili ya zambi na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kuteketezea sadaka. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka.


Kuhani atatwaa sehemu ya damu na kuipakaa kwenye pembe za mazabahu ya kufukizia ubani wenye harufu nzuri, mbele ya Yawe katika hema la mukutano. Damu inayobaki ataimwanga chini kwenye tako la mazabahu ya kuteketezea sadaka inayokuwa karibu na mulango wa hema la mukutano.


Musa akamuchinja huyo ngombe, akatwaa damu akapakaa pembe za mazabahu pande zote kwa kidole chake kwa kuitakasa. Kisha akatwaa damu iliyobaki akaimwanga chini kwenye tako la mazabahu ambayo alitakasa kwa kuifanyia ibada ya upatanisho.


Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.


Wao walioshugulika na kazi ya kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, mazabahu, vyombo makuhani wanavyotumia hema takatifu na pazia; kazi zote zilizoelekea vitu hivi zilikuwa zao.


Basi kuna mambo mawili, ahadi na kiapo, yasiyoweza kubadilika, na kuelekea hayo, Mungu hawezi kusema uongo. Kwa hivi, sisi tuliomukimbilia tunatiwa moyo sana na kushika kwa nguvu tumaini tulilowekewa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ