Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 26:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa makerubi waliochorwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 26:1
29 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

mufalme Daudi akamwambia nabii Natani: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba iliyojengwa na miti ya mierezi, lakini Sanduku la Mungu linakaa ndani ya hema.”


Kuta za kila chumba alizipamba kwa kuchongwa michoro ya makerubi, miti ya ngazi na michoro ya maua yaliyochanua.


Wakati mufalme Daudi alipokuwa akiikaa katika nyumba yake ya kifalme, siku moja akamwita nabii Natani, na kumwambia: “Angalia, mimi ninakaa katika nyumba nzuri iliyojengwa na miti ya mwerezi, lakini Sanduku la Agano la Yawe linakaa ndani ya hema.”


Hema la Yawe ambalo lilitengenezwa na Musa katika jangwa, na mazabahu ya sadaka ya kuteketezwa, wakati ule vilikuwa bado pale pahali pa kuabudia kule Gibeoni.


Utatengeneza vilevile mufano wa makerubi wawili kwa kufua zahabu, uwaweke kwenye miisho miwili ya kiti kile;


sufu ya samawi, ya zambarau na nyekundu, kitani safi iliyosokotwa na manyoya ya mbuzi;


Vilevile Waisraeli watanitengenezea hema takatifu, kusudi niweze kukaa kati yao.


Kila pazia litakuwa na urefu wa metre kumi na mbili na upana wa metre mbili. Mapazia hayo yakuwe ya kipimo kimoja.


Utatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya samawi, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Juu ya pazia lile utachora kwa ufundi sanamu za makerubi.


Kwa ajili ya mulango wa hema utatengeneza pazia zito kwa sufu ya rangi ya samawi, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kuchorwa vizuri.


hema la mukutano, Sanduku la Agano na kiti cha ushuhuda juu yake, pamoja na vifaa vyake vyote,


kutengeneza hema takatifu, kifuniko chake na pazia lake, vifungio vyake, miti yake, vikalio vyake;


Amewapa ujuzi wa kufanya kila kazi ya ufundi au inayofanywa na watu wa akili au wafundi wa kushona kwa sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau, nyekundu na kitani safi iliyosokotwa kwa kutumia ufundi wowote wa akili.


sufu ya samawi, ya zambarau na nyekundu; kitani safi iliyosokotwa; manyoya ya mbuzi;


Alitengeneza pazia la nyuzi za rangi ya samawi, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Pazia hilo lilipambwa na makerubi kwa ufundi.


Wakafua zahabu na kuikata katika nyuzi nyembamba kwa kuzifuma pamoja na sufu ya rangi ya samawi, ya zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa kwa ufundi.


Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, utasimika hema takatifu la mukutano.


Kazi ya wana wa Gersoni ilikuwa kutunza hema takatifu, hema pamoja na kifuniko chake, pazia la mulango wa hema la mukutano,


watabeba mapazia ya hema takatifu na hema la mukutano pamoja na kifuniko chake, kifuniko cha ngozi laini ya mbuzi kinachokuwa juu yake, pazia la mulango,


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Lakini hekalu ambalo Yesu alisema juu yake lilikuwa mwili wake.


Yeye anafanya kazi ya Kuhani Mukubwa katika Pahali Patakatifu Sana, maana yake katika hema ya kweli iliyosimikwa na Bwana, wala si mutu.


Kufuatana na ile, kulikuwa Hema iliyosimikwa. Chumba chake cha kwanza kiliitwa Pahali Patakatifu. Ndani ya chumba kile kulikuwa kinara cha kuwekea taa, meza na mikate iliyotolewa kwa Mungu.


Huo ni mufano wa wakati wa sasa unaoonyesha kwamba matoleo na sadaka zinazotolewa kwa Mungu haziwezi kumufanya yule anayeabudu kuwa na moyo mukamilifu.


Yule bibi amepewa nguo ya kuvaa iliyofumwa na nyuzi nzuri zenye kungaa. (Nguo ile ni mufano wa matendo ya haki ya watu wa Mungu.)


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ