Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 24:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Musa akatwaa ile damu na kuwanyunyizia watu, akisema: Hii ndiyo damu ya agano ambalo Yawe amefanya nanyi kufuatana na maneno haya yote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 24:8
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Zaidi ya hayo, nimetenga nafasi ya kuweka Sanduku la Agano ambalo ndani yake muko agano Yawe alilofanya na babu zetu, wakati alipowatoa katika inchi ya Misri.”


Hakukukuwa kitu ndani ya Sanduku la Agano lakini vile vibao viwili vya mawe ambavyo Musa aliviweka mule kule Horebu, pahali Yawe alipofanya agano na Waisraeli walipotoka katika inchi ya Misri.


Lakini walimudanganya kwa maneno yao; walimwambia uongo.


Musa akachota nusu ya damu ya nyama wale na kuiweka katika mabeseni na nusu ingine akainyunyiza juu ya mazabahu ile.


Lakini sasa ameyashangaza mataifa mengi. Wafalme watapumbazika kwa sababu yake, maana wataona mambo ambayo hawajapata kuambiwa, na kufahamu mambo ambayo hawajapata kusikia.


Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.


Nilipopita tena karibu nawe, nikakuona. Wakati huu, ulikuwa umefikia umri wa kupendwa kama binti. Nikalitandaza vazi langu juu yako na kuufunika uchi wako. Nikafanya nawe agano la ndoa, nawe ukakuwa wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Halafu Musa akatwaa mafuta ya kupakaa na damu kutoka mazabahu akamunyunyizia Haruni na wana wake hata na nguo zao vilevile. Hivyo Musa akamutakasa Haruni na wana wake pamoja na nguo zao.


Mulipotoka Misri niliwaahidi kwamba nitakuwa pamoja nanyi siku zote. Basi, ningali pamoja nanyi, kwa hiyo, musiogope kitu.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya agano langu pamoja nanyi, agano lililokamilishwa kwa njia ya damu, nitawakomboa wafungwa wenu wanaokuwa kama wamefungwa katika shimo tupu.


kwa maana hii ni damu yangu inayomwangika kwa ajili ya wengi kusudi wasamehewe zambi. Nayo damu hii inahakikisha agano la Mungu.


Na Yesu akawaambia: “Hii ni damu yangu; damu inayomwangika kwa ajili ya watu wengi kwa kuhakikisha agano la Mungu.


Vilevile kisha kula akatwaa kikombe na kuwapa akisema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu.]


Vilevile, nyuma ya kula akatwaa kikombe na kusema: “Kikombe hiki ni agano jipya la Mungu, linalohakikishwa kwa njia ya damu yangu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka kila mara munapokikunywa.”


Kwa njia ya damu ya Kristo, sisi tumekombolewa, maana yake zambi zetu zimesamehewa. Hivi Mungu ameonyesha uwingi wa neema yake


Yawe, Mungu wetu, alifanya agano nasi kwenye mulima Horebu.


Basi munazania itakuwa namna gani? Hataazibiwa vikali zaidi yule anayemuzarau Mwana wa Mungu na kuihesabu kuwa bure damu ya agano la Mungu iliyomutakasa na kumutukana Roho wa neema?


Mungu wa amani, aliyemufufua Bwana wetu Yesu ambaye ni Muchungaji mukubwa wa kondoo kwa njia ya kumwanga damu yake inayohakikisha agano la milele,


Hivyo, Yoshua akafanya agano na Waisraeli kule Sekemu, akawapa masharti na maagizo ya kufuata.


Mungu Baba aliwachagua ninyi tangu mbele kufuatana na mupango wake na kufanywa watakatifu na Roho, mupate kumutii Yesu Kristo na kusafishwa kwa damu yake. Ninawatakia neema na amani kwa uwingi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ