Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 24:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Musa akaandika maagizo yote ambayo Yawe alimupa. Kisha akaamuka asubui mapema, akajenga mazabahu chini ya mulima na kusimamisha nguzo kumi na mbili kulingana na hesabu ya makabila kumi na mbili ya Israeli.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 24:4
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Yawe akamutokea Abramu, akamwambia: “Nitawapa wazao wako inchi hii.” Basi, Abramu akajenga mazabahu kwa ajili ya Yawe aliyemutokea.


Yakobo akaamuka asubui mapema, akatwaa lile jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake, akalisimika kama nguzo na kulitakasa kwa kulimiminia mafuta.


Nalo jiwe hili nililosimika hapa kama nguzo, litakuwa nyumba yako Mungu, nami nitakupa sehemu ya kumi ya vitu vyote utakavyonipa.”


Basi, Yakobo akatwaa jiwe, akalisimika kama nguzo ya ukumbusho.


Mara moja, Ahiya akavua nguo yake mupya, akaipasua kwa vipande kumi na viwili,


Alitwaa mawe kumi na mawili, hesabu ya makabila kumi na mawili yaliyopewa majina ya wana wa Yakobo ambaye neno la Yawe lilimufikia kusema hivi: “Jina lako litakuwa Israeli.”


Wakati wa kuizindua nyumba ya Mungu, walitoa ngombe dume mia moja, kondoo dume mia mbili, wana-kondoo mia ine na beberu kumi na wawili kwa ajili ya sadaka ya kusamehewa zambi, mbuzi mumoja kwa kila kabila la Israeli.


Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara kwa maandiko na wakubwa wetu, Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na muhuri wao.


Kisha Yawe akamwambia Musa: “Uandike jambo hili katika kitabu, likuwe ukumbusho. Tena umwambie Yoshua kwamba nitawafuta kabisa Waamaleki katika dunia.”


Musa akajenga mazabahu na kuita mazabahu hiyo “Yawe ni Bendera Yangu”,


Kisha akatwaa kitabu cha agano la Yawe, akakisoma mbele ya watu, nao wakasema: Yale yote Yawe aliyoyasema tutayafanya, nasi tutakuwa watiifu.


Basi, kutakuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama muhuri, kwa kusimamia makabila yale kumi na mawili.


Yawe akamwambia Musa: Andika maneno haya, maana kulingana na maneno haya, ninafanya agano nawe na watu wa Israeli.


Siku hiyo, kutakuwa mazabahu kwa ajili ya Yawe katikati ya inchi ya Misri, na nguzo iliyotakaswa kwa ajili ya Mungu kwenye mpaka wa Misri.


Twaa unga laini, kilo kumi na mbili na kupika mikate kumi na miwili.


Umwambie Eleazari mwana wa kuhani Haruni atoe hivyo vyetezo kwenye moto, atupe mbali moto unaokuwa ndani, maana vyetezo hivyo ni vitakatifu.


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Basi Yakobo, Petro na Yoane, waliohesabiwa kuwa waongozi wakubwa, walitambua neema ile niliyojaliwa na Mungu wakatupatia mukono, mimi na Barnaba kuwa kitambulisho cha ushirika. Hivi tukapatana kwamba sisi tutakwenda kuhubiri watu wa mataifa mengine na wao watakwenda kuhubiri Wayuda.


Basi, Musa akaandika sheria hiyo, akawapa makuhani wa ukoo wa Lawi ambao walikuwa wakibeba Sanduku la Agano la Yawe, na wazee wote wa Israeli.


Yoshua akayasimika yale mawe kumi na mawili ambayo waliyatwaa kutoka muto Yordani, kule Gilgali.


akawaambia: “Mulitangulie Sanduku la Agano la Yawe, Mungu wenu, mpaka katikati ya muto Yordani. Kila mumoja wenu abebe jiwe kwenye bega lake, jiwe moja kwa ajili ya kila kabila la Israeli.


Na ukuta uliozunguka muji ule ulikuwa umejengwa juu ya mawe ya musingi kumi na mawili na juu ya kila jiwe kulikuwa kumeandikwa jina la kila mumoja wa mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ