Mutu akiwakulishia nyama wake katika shamba la mizabibu au kumwachilia nyama wake kula katika shamba la mutu mwingine, atalipa hasara ile kwa mazao bora ya shamba lake mwenyewe au shamba lake la mizabibu.
Umupatie Haruni na wana wake maagizo haya: hii ndiyo sheria ya ibada juu ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto. Sadaka ya kuteketezwa itakuwa kwenye moto juu ya mazabahu usiku kucha mpaka asubui na moto wake uchochewe, usizimike.
Moto wa mazabahu lazima uendelee kuwaka wala usizimike. Kila siku asubui kuhani ataweka kuni kwenye moto huo na juu yake atapanga sadaka ya kuteketezwa, mbele ya kuteketeza mafuta ya sadaka ya amani.
(Hakusema maneno haya kwa sababu aliwasikilia wamasikini huruma, lakini kwa sababu alikuwa mwizi. Ni yeye aliyekuwa akichunga mufuko wa feza, naye alikuwa akijitwalia mali toka ndani yake.)