Kutoka 22:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Mutu akimwachia mwenzake feza au mali nyingine amutunzie, kisha ikaibiwa ndani ya nyumba yake, mwizi akipatikana anapaswa kulipa bei yake mara mbili.
Kama yule nyama aliraruliwa na nyama wa pori, yule mutu aliyekuwa amepewa anapaswa kumuleta kama ushuhuda. Hatalipa malipo yoyote kwa ajili ya nyama aliyeraruliwa na nyama wa pori.
Mutu akiwasha moto nao ukichoma miti ya miiba na kusambaa mpaka kuteketeza miganda ya ngano au ngano ya mutu mwingine ambayo bado haijavunwa au shamba lote likiteketea, aliyewasha moto ule anapaswa kulipa hasara ile yote.