Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 21:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Ukimununua mutumwa Mwebrania, atakutumikia kwa miaka sita, lakini mwaka wa saba atakuwa huru na kuondoka, bila malipo.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 21:2
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akumiminie umande wa mbinguni, akupe udongo wenye mboleo, ngano na divai kwa wingi.


Esau akasema: “Ndiyo maana anaitwa Yakobo! Ametwaa nafasi yangu mara mbili. Kwanza alitwaa haki yangu ya muzaliwa wa kwanza, na sasa ametwaa baraka yangu.” Kisha akamwuliza baba yake: “Basi, haukuniwekea baraka yoyote?”


Basi, mwanamuke mumoja kati ya wake za wanafunzi wa manabii akamwendea Elisha, akamwambia: “Mutumishi wako, mume wangu amekufa, na kama vile unavyojua, alikuwa mwenye kumwogopa Mungu. Lakini mutu aliyemukopesha feza amekuja kuwatwaa wana wangu wawili wakuwe watumwa wake.”


Nikasema: “Kulingana na uwezo tunaokuwa nao, tumekuwa tukiwanunua tena wandugu zetu Wayuda waliokuwa wameuzishwa kwa watu wa mataifa mengine. Lakini sasa hata munawauzisha wandugu zenu, nasi tunalazimika kuwanunua!” Basi wakanyamaza kimya, bila kuwa na la kujibu.


Lakini mutumwa yeyote aliyenunuliwa kwa feza, nyuma ya kumutahiri, ataruhusiwa kushiriki.


Kama alinunuliwa mbele hajaoa, ataondoka peke yake. Lakini kama alikuja na muke wake, basi, ataondoka na muke wake.


Mutu akimwuzisha binti yake kuwa mujakazi, yule hatapata uhuru wake kama watumwa wanaume.


Kama nyama aliyeibwa, akuwe ni ngombe, punda au kondoo, akipatikana muzima kwa mwizi, basi, yule mwizi atalipa nyama wawili.


Lakini ikiwa mutu huyu na jamaa yake hakukombolewa kwa njia hizo, basi apewe uhuru wake katika mwaka wa ukumbusho wa miaka makumi tano.


Na kwa kuona mutumishi yule hakukuwa na jinsi ya kulipa deni lile, bwana wake akaamuru auzishwe kuwa mutumwa, yeye na muke wake pamoja na watoto wake na vyote alivyokuwa navyo viuzishwe vilevile, kusudi apate kumulipa.


Kwa sababu mulinunuliwa na Mungu kwa bei kali. Basi mutumie miili yenu na roho zenu kwa utukufu wa Mungu.


“Kila mwisho wa mwaka wa saba mutawasamehe wote wenye kuwa na madeni yenu.


Wala usione ugumu utakapomwacha huru mutumwa wako, maana, amekutumikia kwa muda wa miaka sita kwa nusu ya mushahara wa mutumishi wa kulipwa. Fanya hivyo, naye Yawe, Mungu wako, atakubariki kwa kila utakalofanya.


Kisha akawaamuru akasema: “Kila mwaka wa saba utakuwa mwaka wa mafungulio. Katika sikukuu ya vibanda, mwaka huo,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ