Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 20:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Usisahau kuiweka takatifu siku ya Sabato.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 20:8
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mushike Sabato zangu na kuheshimu Pahali pangu Patakatifu. Mimi ni Yawe.


Kila mumoja wenu anapaswa kuheshimu mama yake na baba yake, na kushika Sabato zangu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mungu akaibariki siku ya saba na kuitakasa, maana kwa siku hiyo Mungu alipumzika kisha kazi yake yote ya kuumba.


Kutakuwa siku sita za kufanya kazi. Lakini siku ya saba ni Sabato. Siku hiyo ni ya mapumziko, hamutafanya kazi na mutakuwa na mukutano mutakatifu. Siku hiyo ya saba hamutafanya kazi. Hiyo ni Sabato ambayo ni takatifu kwangu mimi Yawe katika makao yenu yote.


Mutashika Sabato zangu na kuheshimu Pahali pangu Patakatifu. Mimi ni Yawe.


Kwa siku sita utafanya kazi zako, lakini siku ya saba utapumzika, kusudi ngombe wako na punda wako vilevile wapate kupumzika, na watoto wa mujakazi wako na wageni wapate kustarehe.


Kwa siku ya saba Mungu alikuwa amemaliza kazi yake yote aliyofanya. Kwa siku ile ya saba Mungu akapumzika kisha kazi yake yote aliyofanya.


“Shika siku ya Sabato na kuitakasa, kama vile mimi Yawe, Mungu wako, nilivyokuamuru.


Kwa njia ya Musa, mutumishi wako, ukawajulisha siku zako za Sabato takatifu na ukawaagiza kuzifuata amri, masharti na sheria ulizowaamuru.


Wakati uleule, nikawaona watu wa Yuda wakikamua zabibu katika vikamulio siku za Sabato. Tena wengine walikuwa wakiwabebesha punda wao ngano, divai, zabibu, tini na vitu vingine wakivipeleka Yerusalema. Nikawaonya kwamba hawana ruhusa ya kuuzisha katika siku hiyo.


Heri mutu anayefuata maneno hayo, anayeshika kabisa siku za Sabato kwa heshima na kuepuka kutenda uovu wowote.


Musibebe muzigo kutoka nyumba zenu siku ya Sabato wala kufanya kazi yoyote. Lakini muihesabu siku ya Sabato kuwa takatifu kama nilivyowaamuru babu zenu.


Lakini ninyi munisikilize mimi. Muache kuingiza muzigo wowote kupitia kwenye milango ya muji huu siku ya Sabato, muihesabu kuwa takatifu na kutofanya kazi.


Musa akakusanya Waisraeli wote pamoja, akawaambia: Haya ndiyo mambo ambayo Yawe amewaamuru kufanya:


Siku moja, wakati Waisraeli walipokuwa katika jangwa, wakamwona mutu mumoja akiokota kuni siku ya Sabato.


Kama ukiacha kufanya kazi siku ya Sabato, ukiacha shuguli zako siku yangu hiyo takatifu, ukiifanya siku yangu kuwa ya furaha, ukiheshimu siku hiyo takatifu ya Yawe, ukiacha shuguli zako au kupiga domo,


Uwaambie kwamba: Yawe anasema hivi: Mufanye angalisho kwa ajili ya maisha yenu. Musibebe muzigo siku ya Sabato, au kuingiza muzigo katika Yerusalema kupitia kwenye milango ya muji.


Mufanye Sabato zangu kuwa takatifu, kusudi zikuwe kitambulisho cha agano langu nanyi. Hizo zitawakumbusha kwamba mimi Yawe ni Mungu wenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ