Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 20:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Usijifanyie sanamu ya miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 20:4
41 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”


na walitumikia sanamu ambazo Yawe alikuwa amewakataza, akisema: “Musifanye hivyo.”


Nayo sanamu aliyotengeneza, akaiweka katika nyumba ya Mungu ambayo aliizungumuzia, mbele ya Daudi na mwana wake Solomono: “Katika nyumba hii na katika Yerusalema kati ya makabila kumi na mawili ya Israeli, ndipo pahali nitakapoabudiwa milele.


Walimukasirikisha kwa mazabahu zao za miungu; wakamutia wivu kwa sanamu zao za kuchongwa.


Wote wanaoabudu sanamu na kujisifia miungu ya bure wanafezeheshwa. Miungu yote inainama mbele yake.


Mutaniheshimu mimi peke yangu wala musijifanyie miungu ya feza wala ya zahabu.


Watu walipoona kwamba Musa amechelewa kurudi kutoka juu ya mulima, wakakusanyika mbele ya Haruni na kumwambia: Basi! Ututengenezee miungu itakayotuongoza, maana hatujui jambo lililomupata yule Musa aliyetutoa katika inchi ya Misri.


Walikuja wakaniambia: Utufanyie miungu ambayo itatuongoza, maana yule Musa aliyetutoa katika inchi ya Misri hatujui jambo lililomupata.


Naye akazitwaa akaziyeyusha, akatengeneza sanamu ya mwana-ngombe. Watu wakapaaza sauti wakasema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri.


Wameacha mara moja njia niliyowaamuru, wakajifanyia sanamu ya mwana-ngombe, nao wamemwabudu na kumutolea sadaka wakisema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri!


Wote wanaotegemea sanamu za miungu, wote wanaoziambia “Ninyi ni miungu yetu” watakomeshwa na kupata haya.


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Watengenezaji wa sanamu watapata haya na kuzarauliwa, wote pamoja watafezeheka.


Niliwaambia: Mutupilie mbali machukizo yote munayoyapenda; musijichafue na sanamu za miungu ya Misri, kwa maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Basi, nikaingia, nikaona vitu vya kuchukiza vimechorwa kuzunguka ukuta: kila aina ya nyama wanaotambaa, vidudu, na sanamu zote za miungu ya Waisraeli.


Basi, akanyoosha kitu kinachokuwa kama vile mukono, akanikamatia kwa nywele zangu. Roho wa Mungu akaninyanyua kati ya dunia na mbingu, akanipeleka mpaka Yerusalema nikiwa katika maono hayo ya Mungu. Nikafika kwenye kiingilio cha mulango wa baraza ya ndani inayoelekea upande wa kaskazini, pahali palipowekwa sanamu iliyomuletea Mungu wivu.


Musigeukie sanamu za miungu, wala musijitengenezee sanamu za kuyeyushwa za miungu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Musijitengenezee sanamu za miungu ya uongo, musishike sanamu zao za kuchongwa wala nguzo wala sanamu za mawe yaliyochongwa katika inchi yenu na kuviabudu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mimi ninaongea naye kinywa kwa kinywa, waziwazi na si kwa kutumia mafumbo. Yeye ameliona umbo langu mimi Yawe. Kwa nini, basi, hamukuogopa kusema vibaya juu ya mutumishi wangu Musa?


Basi kwa kuwa sisi tuko watoto wa Mungu, tusiwaze kwamba anafanana na sanamu ya zahabu au ya feza au ya jiwe, iliyochorwa kwa ufundi na akili ya watu.


Kwa pahali pa kumwabudu Mungu anayeishi milele, wakaabudu sanamu zilizochongwa kwa mufano wa mutu anayekufa, wa ndege, wa nyama na hata viumbe vyenye kutambaa.


Wala musisimamishe nguzo ambayo Yawe Mungu wenu anaichukia.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayefanya sanamu ya kuchonga au ya kuyeyushwa na kuisimamisha kwa siri, kitu ambacho kimetengenezwa na mikono ya fundi na ambacho ni chukizo kwa Yawe, Mungu wenu’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


“Usijifanyie sanamu za miungu, wala mufano wa kitu chochote kinachokuwa juu mbinguni, wala kinachokuwa chini katika dunia, wala kinachokuwa ndani ya maji chini ya dunia.


Malaika wa kwanza akamwanga kikombe chake katika dunia. Halafu majipu mabaya na yenye kuumiza sana yakaota juu ya watu waliokuwa na chapa ya yule nyama na walioabudu sanamu yake.


Watu waliobaki bila kuuawa na yale mapigo hawakuachana na sanamu walizojitengenezea wao wenyewe. Hawakuacha kuabudu pepo, sanamu za zahabu, za feza, za shaba, za mawe na za miti zisizoweza kuona, wala kusikia, wala kutembea.


Mika akamurudishia mama yake hivyo vikoroti vya feza elfu moja na mia moja. Mama yake akasema: “Kusudi laana niliyotoa isikupate, feza hii ninaitoa kwa Yawe kwa kutengeneza sanamu ya kuchonga na ya kuyeyushwa. Sasa ninakurudishia vikoroti vya feza.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ