Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 20:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Usikuwe na miungu mingine isipokuwa mimi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 20:3
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana, alipokuwa muzee, wake zake walimupotosha hata akaitumikia miungu mingine, wala hakukuwa mwaminifu kabisa kwa Yawe, Mungu wake, kama baba yake Daudi alivyokuwa mwaminifu.


Museme kwamba jina la Yawe ni tukufu. Mumwabudu katika pahali pake patakatifu.


Mbinguni, nani anayeweza kunisaidia isipokuwa wewe? Na katika dunia hamuna ninachokitamani isipokuwa wewe!


Usikuwe na mungu wa kigeni; usiabudu hata kidogo mungu mwingine.


Enyi watu wangu, musikie onyo langu. Heri ungenisikiliza, ee Israeli!


“Ewe Yawe, ni nani kati ya miungu anayelingana nawe? Ni nani aliyekuwa kama wewe unayekuwa mutakatifu mukubwa, unayetisha kwa matendo matukufu, unayetenda mambo ya ajabu?


Mutaniheshimu mimi peke yangu wala musijifanyie miungu ya feza wala ya zahabu.


Anayemutolea mungu mwingine sadaka pahali pa Yawe pekee, lazima aangamizwe kabisa.


Musiiname mbele ya miungu yao kuiabudu, wala kuitumikia, wala musiige mambo yao. Lakini mutawaangamiza kabisa na kuvunjavunja nguzo zao.


Wameacha mara moja njia niliyowaamuru, wakajifanyia sanamu ya mwana-ngombe, nao wamemwabudu na kumutolea sadaka wakisema: Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa katika inchi ya Misri!


Musiabudu mungu yeyote mwingine, maana mimi Yawe ninajulikana kwa jina: Mwenye Wivu. Mimi ni Mungu mwenye wivu.


Mutumainie Yawe siku zote kwa maana yeye ni kikingio chetu kwa milele.


Jina langu mimi ni Yawe; sitamupa mwingine utukufu wangu, wala sifa zangu sanamu za miungu.


Ninyi Waisraeli ni washuhuda wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.– Niliwachagua mukuwe watumishi wangu, mupate kunijua na kuniamini, kwamba mimi ni Mungu. Mbele yangu hakukuwa mungu mwingine, wala hakutakuwa mungu mwingine nyuma yangu.


Enyi watu wangu, musiogope wala musikuwe na hofu, Sikuwaambia tangu zamani mambo yatakayotokea? Ninyi ni washuhuda wangu. Kuna mungu mwingine isipokuwa mimi? Kuna mwenye nguvu mwingine? Yule simujui!


Mukumbuke mambo niliyotenda hapo zamani! Mimi ni Mungu. Hakuna Mungu mwingine. Mimi ni Mungu. Hakuna mwingine kama mimi.


Musifuate miungu mingine wala kuitumikia na kumukasirikisha kwa kuabudu sanamu, nami sitawatendea ubaya wowote.


Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.


Munaiba, munaua, munafanya uzinzi, munaapa kwa uongo, munamufukizia mungu Bali ubani na kuabudu miungu mingine ambayo hamujapata kuijua.


Lakini, hata kama haitafanyika hivyo, ujue wazi, ee mufalme, kwamba sisi hatutaitumikia miungu yako wala kuiabudu sanamu ya zahabu uliyosimamisha.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Lakini Yesu akamwambia: “Toka wewe, Shetani! Kwa maana imeandikwa: ‘Umwabudu Bwana Mungu wako na umutumikie yeye peke yake.’ ”


Basi kuelekea lile ulizo juu ya kula nyama za kutambikiwa kwa sanamu za miungu, tunajua kwamba sanamu ni kitu bure katika dunia, na ya kuwa kuna Mungu mumoja peke yake tu.


Ingawa hivi, kwa ngambo yetu sisi tuko na Mungu mumoja peke yake tu, ndiye Baba aliyeumba vitu vyote, nasi tunaishi kwa nguvu yake. Vilevile kuko Bwana mumoja tu, ndiye Yesu Kristo. Kwa njia yake vitu vyote viliumbwa, nasi tunaishi kwa nguvu yake.


Mujue waziwazi kwamba mwasherati yeyote na muchafu na mwenye tamaa ya mali (mwenye tamaa ni kama mwenye kuabudu sanamu), hao wote hawatapewa sehemu ya urizi katika Ufalme wa Kristo na Mungu.


Musiabudu miungu mingine, miungu ya watu wanaokuwa jirani nanyi,


Mumupende Yawe, Mungu wenu, kwa moyo wenu wote, kwa roho yenu yote na kwa nguvu yenu yote.


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Musikubali kuhukumiwa na mutu yeyote anayejionyesha kwa inje kuwa yeye ni munyenyekevu na mwenye kuabudu malaika. Mutu wa namna hii anatia sana maana juu ya maono anayopata, naye anajitapa bure juu ya mafikiri yake ya kimutu.


Nikaanguka mbele yake kusudi nimwabudu, lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe na wandugu zako wanaoshika ukweli ulioshuhudiwa na Yesu. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu! Maana ukweli ambao Yesu alishuhudia, ndio uwezo unaowaongoza manabii.”


Lakini akaniambia: “Angalia, usifanye vile! Kwa maana mimi ni mutumishi kama vile wewe, na wandugu zako manabii na watu wanaoshika maneno ya unabii yanayoandikwa katika kitabu hiki. Ni Mungu ndiye unayepaswa kumwabudu!”


Kisha nikawakumbusha kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, na kwamba musiiheshimu miungu ya Waamori, ambao inchi yao mumeitwaa, lakini hamukuisikiliza sauti yangu.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ