Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 20:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 20:2
50 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu walipoona hivyo, walianguka uso mpaka chini na kusema: “Yawe ndiye Mungu! Yawe ndiye Mungu!”


na walitumikia sanamu ambazo Yawe alikuwa amewakataza, akisema: “Musifanye hivyo.”


Haya yote yalitendeka kwa sababu watu wa Israeli walimwasi Yawe, Mungu wao, ambaye aliwatoa kutoka mikono ya mufalme wa Misri, vilevile waliabudu miungu mingine,


Yawe, Mungu wake akamwacha mufalme Ahazi ashindwe na mufalme wa Suria ambaye vilevile akawapeleka watu wake wengi, akarudi nao Damasiki. Vilevile, alimufanya ashindwe na mufalme wa Israeli ambaye alimushinda na kuua watu wengi sana.


“Enyi watu wangu, munisikilize, mimi Mungu, Mungu wenu! Ninataka kusema nanyi. Israeli, ninakuonya.


Usikuwe na mungu wa kigeni; usiabudu hata kidogo mungu mwingine.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri. Fungua kinywa chako, nami nitakulisha.


“Mimi nilikutua mizigo yako toka kwenye mabega, nilikuondolea matofali uliyochukua katika mikono.


Kama kisha mwana wako akiuliza maana ya jambo hili, utamwambia: ‘Kwa nguvu ya mukono wake, Yawe alitutoa katika inchi ya Misri ambako tulikuwa watumwa.


Musa akawaambia watu: “Mukumbuke siku hii muliyotoka inchi ya Misri ambako mulikuwa watumwa. Hii ndiyo siku Yawe alipowatoa humo kwa mukono wake wenye nguvu. Katika siku hii, musikule mukate uliotiwa chachu.


“Kwa wema wako mukubwa umewaongoza watu uliowakomboa, kwa nguvu yako umewaongoza kwenye makao yako matakatifu.


Kitisho na hofu vimewashika. Kwa sababu ya ukubwa wa nguvu zako, wao wamenyamaza kimya kama jiwe, mpaka watu wako, ee Yawe, wapite, mpaka watu wale uliowakomboa wamewapita.


akawaambia: “Ikiwa mutaisikiliza kwa uaminifu sauti yangu mimi Yawe, Mungu wenu, kutenda yale yanayokuwa sawa mbele yangu, na kuheshimu amri na masharti yangu yote, basi, mimi sitawaletea yale magonjwa niliyowaletea Wamisri. Kwa sababu, mimi ni Yawe ninayewaponya ninyi.”


Hapo ndipo watakapotambua kwamba mimi ni Yawe, Mungu wao, niliyewaleta kutoka katika inchi ya Misri, kusudi niishi kati yao. Mimi ni Yawe, Mungu wao.


Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.


Maana mimi ni Yawe, Mungu wenu, Mungu Mutakatifu wa Israeli, Mwokozi wenu. Ninaitoa inchi ya Misri kwa ajili ya ukombozi wenu, ninaitoa Kushi na Seba kusudi muachwe huru.


Kwa hiyo, siku zinakuja ambapo watu hawataapa tena wakisema: Kama vile Yawe anavyoishi, yule aliyewaondoa Waisraeli kutoka inchi Misri.


Hawakujiuliza hivi: Yuko wapi Yawe aliyetuondoa katika inchi ya Misri, aliyetuongoza katika mbuga, katika inchi ya jangwa na mashimo, inchi inayokauka na yenye giza kubwa, inchi isiyopitiwa na mutu yeyote, wala kukaliwa na mwanadamu?


Kutakuja siku ambazo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Waisraeli, nao watakuwa watu wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Nilifanya agano na babu zenu nilipowatoa toka inchi ya Misri ambako walikuwa watumwa, nikawaambia:


Mimi Yawe ni Mungu wenu. Mufuate masharti yangu, mushike maagizo yangu kwa uangalifu.


Uwaambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Siku ile nilipowachagua Waisraeli niliwaapia wazao wa Yakobo. Nilijijulisha kwao katika inchi ya Misri, nikawaapia nikisema: Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Niliwaambia: Mutupilie mbali machukizo yote munayoyapenda; musijichafue na sanamu za miungu ya Misri, kwa maana mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Yawe anasema: Mimi ni Yawe, Mungu wako, tangia katika inchi ya Misri! Mimi nitakukalisha tena katika mahema, kama vile mulivyofanya wakati nilipokutana nanyi.


Yawe anasema: Lakini mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri; hakuna mungu mwingine lakini mimi, wala hakuna anayeweza kuwaokoa.


Kwa sababu ni mimi Yawe niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi nikuwe Mungu wenu; kwa hiyo mukuwe watakatifu kwa maana mimi ni mutakatifu.


Munapaswa kutumia mizani ya kweli na vipimo vinavyokuwa vya kweli. Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri.


Jambo hilo litajulisha vizazi vyenu kwamba nilipowatoa babu zenu katika inchi ya Misri, niliwafanya waishi katika vibanda. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyekutoa kutoka inchi ya Misri kwa kukupa inchi ya Kanana, na kusudi nami nikuwe Mungu wako.


Kwa sababu Waisraeli ni watumishi wangu ambao niliwatoa katika inchi ya Misri, basi, wasiuzishwe kama watumwa.


Waisraeli ni watumishi wangu, maana niliwatoa katika inchi ya Misri. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Musijitengenezee sanamu za miungu ya uongo, musishike sanamu zao za kuchongwa wala nguzo wala sanamu za mawe yaliyochongwa katika inchi yenu na kuviabudu. Mimi ni Yawe, Mungu wenu.


Mimi ni Yawe, Mungu wenu, niliyewatoa katika inchi ya Misri kusudi musikuwe watumwa wa Wamisri. Mimi nimevunja nira muliyofungiwa katika shingo lenu na kuwafanya mutembee wima.


Niliwatoa ninyi kutoka inchi ya Misri, nikawaongoza kupitia katika jangwa miaka makumi ine, mpaka mukaitwaa inchi ya Waamori kuwa yenu.


Basi hakuna tofauti kati ya Wayuda na watu wa mataifa mengine, kwa maana Bwana wa wote ni mumoja tu, na anawabariki sana wote wanaomusihi.


Au Mungu ni Mungu wa Wayuda tu? Yeye si Mungu wa watu wa mataifa mengine vilevile? Ndiyo, yeye ni Mungu wa watu wa mataifa mengine vilevile,


lakini utamwua. Mukono wako unapaswa ukuwe wa kwanza wakati wa kumwua halafu wengine wote watafuata vilevile.


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


Usisahau kwamba wewe ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri, nami Yawe, Mungu wako, nikakutoa huko kwa mukono wenye nguvu na mukono ulionyooshwa. Ndiyo maana mimi Yawe, Mungu wako, nimekuamuru kushika siku ya Sabato.


“Mimi ni Yawe, Mungu wako, niliyekutoa katika inchi ya Misri, ambako ulikuwa mutumwa.


Lakini ni kwa sababu Yawe anawapenda na anashika kiapo alichowaapia babu zenu, ndiyo maana aliwaokoa kwa nguvu zake kubwa na kuwaokoa toka katika utumwa, toka mikono ya mufalme wa Misri.


Malaika wa Yawe aliondoka Gilgali, akaenda Bokimu, akawaambia Waisraeli: “Niliwaondoa katika inchi ya Misri na kuwaleta katika inchi ambayo niliahidi kwa kiapo kwa babu zenu. Nilisema kwamba sitalivunja agano langu nanyi hata kidogo.


Kisha nikawakumbusha kwamba mimi ni Yawe, Mungu wenu, na kwamba musiiheshimu miungu ya Waamori, ambao inchi yao mumeitwaa, lakini hamukuisikiliza sauti yangu.’ ”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ