Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.
Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”
Basi, binti ya mufalme wa Misri akashuka kwenye muto kuoga na wajakazi wake wakakuwa wanatembeatembea kandokando ya muto. Binti ya mufalme akaona kile kikapu katika majani, akamutuma mujakazi wake akitwae.