Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Lakini kwa vile hakuweza kumuficha zaidi ya muda ule, akatengeneza namna ya kikapu cha mafunjo, akakipakaa namna ya kabulimbo, akamutia yule mutoto ndani. Kisha akaweka kikapu kando ya muto Nili katika majani.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 2:3
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha wakaambiana: “Tufanye matofali, tuyachome kwa moto vizuri.” Walikuwa na matofali pahali pa mawe, na kabulimbo pahali pa chokaa.


Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya kabulimbo; kwa hiyo wafalme wa Sodoma na Gomora walipokuwa wakikimbia vita, wakatumbukia mule, lakini wengine wakatorokea kwenye mulima.


Kwa hiyo, ujitengenezee chombo kwa mbao ngumu. Gawanya vyumba ndani yake na ukipakae kabulimbo ndani na inje.


Kisha mufalme wa Misri akawaamuru watu wake wote hivi: “Kila mutoto mwanaume atakayezaliwa kwa Waebrania mumutupe ndani ya muto Nili. Lakini kila mutoto mwanamuke, mumwache aishi.”


Inatuma wajumbe ambao wanasafiri ndani ya muto Nili, wamepanda ndani ya mitumbwi iliyotengenezwa na matete. Muende, enyi wajumbe wepesi, kwa taifa kubwa na hodari, la watu warefu wenye ngozi laini, wanaotisha kwa karibu na kwa mbali, taifa la watu wenye nguvu na ushindi, ambalo inchi yake imegawanywa na mito.


Mifereji yake itatoa harufu mbaya, vijito vyake vitapunguka na kukauka. Nyasi na matete yake yataoza.


Muchanga wa moto katika jangwa utakuwa ziwa la maji, inchi kavu itabubujika vijito. Makao ya imbwa wa pori yatajaa maji; nyasi zitaota na kukomaa kama mianzi.


Wale watu wenye elimu walipokwisha kwenda, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto na kumwambia: “Amuka, utwae mutoto pamoja na mama yake na mukimbilie Misri. Mukae kule mpaka nitakapokuambia kwamba urudie, kwa maana Herode anamutafuta mutoto kusudi amwue.”


Herode alipoona kwamba wale watu wenye elimu wamemudanganya, akakasirika sana. Akatuma watu Betelehemu na popote kandokando yake kwa kuua watoto wote waliokuwa na umri wa miaka miwili na chini yake. Alifanya vile kufuatana na jinsi alivyohakikishwa na wale wenye elimu juu ya wakati nyota ilipotokea.


Mufalme huyo akatendea taifa letu kwa udanganyifu, akawatesa babu zetu hata akawalazimisha kuwatupilia watoto wao wachanga kusudi wakufe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ