Kutoka 2:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
2 Basi, mwanamuke yule akapata mimba, akazaa mutoto mwanaume. Alipoona kwamba mutoto yule muchanga alikuwa muzuri, akamuficha kwa muda wa miezi mitatu.
Muke wa Amuramu aliitwa Yokebedi binti ya Lawi, aliyezaliwa Misri. Huyu alimuzalia Amuramu watoto wawili wanaume, Haruni na Musa, na binti mumoja, Miriamu.
Inchi yake ijae yote yanayokuwa mazuri, ibarikiwe kwa huruma wa Yawe, ambaye alitokea katika kichaka. Baraka hizi zishukie watu wa kabila la Yosefu, aliyekuwa mukubwa kati ya wandugu zake.
Kwa njia ya imani wazazi wa Musa walimuficha kwa muda wa miezi mitatu nyuma ya kuzaliwa kwake. Kwa sababu waliona kwamba alikuwa mutoto mwenye sura nzuri, wala hawakuogopa amri ya mufalme.
Hivyo, Yese alituma mutu, naye akaletwa. Yule kijana alikuwa mwenye afya, mwenye macho yenye kungaa na wa kupendeza. Yawe akamwambia Samweli: “Sasa, huyu ndiye; simama umupakae mafuta.”