Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 19:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yawe akamwambia Musa: “Basi, mimi nitakufikia katika wingu zito kusudi Waisraeli wapate kunisikia ninaposema nawe na kukuamini siku zote.” Kisha Musa akamwambia Mungu jinsi watu walivyosema.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 19:9
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu Solomono akasema: “Yawe alisema kwamba atakaa katika giza nene.


Kesho yake, wakaamuka asubui mapema, wakaenda mpaka katika jangwa la Tekoa. Walipokuwa wanaondoka, Yosafati akasimama, akawaambia: “Musikilize, enyi watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema! Mumwamini Yawe, Mungu wenu, nanyi mutakuwa imara. Muwaaminie manabii wake, nanyi mutashinda.”


Halafu Solomono akasema: “Yawe alisema kwamba atakaa katika giza kubwa.


Mawingu na giza nzito vinamuzunguka; haki na sheria ni musingi wa utawala wake.


Alisema nao katika nguzo ya wingu; walitimiza maagizo yake na masharti aliyowapa.


Waisraeli walipoona tendo hilo la ajabu Yawe alilofanya mbele ya Wamisri, wakamwogopa. Wakamwamini Yawe na Musa mutumishi wake.


Basi, siku ya tatu asubui, kukatokea ngurumo na umeme na wingu zito juu ya mulima. Kukasikilika vilevile sauti kubwa ya baragumu ambayo iliwatetemesha watu wote katika kambi.


Watu wote wakasimama mbali wakati Musa alipokaribia lile wingu zito Mungu alimokuwa.


Yawe akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Musa, akataja jina lake: Yawe.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Yawe akamwambia: “Hivyo Waisraeli watapata kuamini kwamba mimi Yawe, Mungu wa baba zao, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo, nimekutokea.”


Ujumbe wa Mungu juu ya inchi ya Misri. Yawe amepanda juu ya wingu linaloenda mbio na kuja mpaka katika inchi ya Misri. Sanamu za miungu ya Wamisri zitatetemeka mbele yake, mioyo ya Wamisri itayeyuka kwa woga.


Hapo Yawe akashuka katika nguzo ya wingu, akasimama kwenye mulango wa hema, akawaita Haruni na Miriamu. Wote wawili wakasogea mbele.


Naye alipokuwa angali akisema, wingu lenye kuangaza likawafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa, ninapendezwa naye sana. Mumusikilize!”


Halafu wingu likatokea na kuwafunika, na sauti ikasikilika toka katikati ya lile wingu ikisema: “Huyu ni Mwana wangu mupendwa. Mumusikilize!”


Yesu akaongeza kuwaambia wanafunzi wake: “Yule anayewasikiliza ninyi, ananisikiliza mimi; yule asiyewapokea ninyi, hanipokei mimi, na yule asiyenipokea mimi, hamupokei yule aliyenituma.”


juu ya siku ile ambayo mulisimama mbele ya Yawe, Mungu wenu, kule Horebu, ndio Sinai, aliponiambia: ‘Muwakusanye hao watu mbele yangu, niwaambie maneno yangu kusudi wajifunze kuniogopa mimi siku zote za maisha yao, na kuwafundisha watoto wao kufanya hivyo’.


Aliwafanya muisikie sauti yake kutoka mbinguni kusudi aweze kuwafundisha; na hapa katika dunia akawafanya muone moto wake mukubwa na kusikia maneno yake kutoka katikati ya moto huo.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ