Kutoka jangwa la Sini, Waisraeli wote pamoja wakasafiri hatua kwa hatua kama vile Yawe alivyoamuru. Watu wakapiga kambi kule Refidimu. Lakini kule hakukukuwa maji ya kunywa.
Yetro, baba mukwe wa Musa, alikuja pamoja na binti yake, ni kusema muke wa Musa, pamoja na watoto. Akamukuta Musa katika jangwa alikokuwa amepiga kambi kwenye mulima wa Mungu.
Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.
Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”
Katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili, mwaka wa pili nyuma ya watu wa Israeli kutoka Misri, Yawe akasema na Musa ndani ya hema la mukutano katika jangwa la Sinai, akamwambia hivi:
Na wakati ule kulipokuwa mukutano wa Waisraeli katika jangwa, yeye alikuwa pale pamoja na babu zetu na yule malaika aliyesema naye kwenye mulima Sinai. Na ni yeye aliyefunuliwa ujumbe wa Mungu unaoleta uzima na kuutangaza kwetu.
Maneno haya ni kama vile mufano: wake hawa wawili ni mufano wa maagano mawili. Yule Hagari, watoto wake waliozaliwa katika hali ya utumwa, ni mufano wa agano lililofanyika kwenye mulima Sinai.