Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 18:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yetro akafurahishwa na yote Yawe aliyotenda kwa ajili ya Waisraeli, kwa kuwaokoa toka katika mikono ya Wamisri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 18:9
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.


Nitakumbusha mema ya Yawe, sifa za Yawe, matendo yake yote kwetu, mambo mazuri aliyowatendea Waisraeli, rehema yake, na wingi wa wema wake.


Mushangilie na kufurahi pamoja na Yerusalema, enyi munaoupenda! Mushangilie pamoja nao, enyi wote mulioulilia!


Mupendane ninyi kwa ninyi kwa kweli kama vile wandugu, nanyi muheshimiane ninyi kwa ninyi.


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Kama kiungo kimoja kikiumia, viungo vingine vyote vinaugua pamoja nacho. Kiungo kimoja kikiheshimiwa, viungo vingine vyote vinafurahi pamoja nacho.


Saulo akawaambia Wakeni: “Muende! Muondoke! Mutoke kati ya Waamaleki, kama sivyo, nitawaangamiza pamoja nao. Muondoke kwa sababu ninyi muliwatendea mema Waisraeli walipotoka Misri.” Basi, Wakeni wakaondoka kati ya Waamaleki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ