Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 18:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Yetro, baba mukwe wa Musa, alikuja pamoja na binti yake, ni kusema muke wa Musa, pamoja na watoto. Akamukuta Musa katika jangwa alikokuwa amepiga kambi kwenye mulima wa Mungu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 18:5
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Elia akaamuka, akakula na kunywa. Kisha akatembea kwa nguvu ya chakula hicho mwendo wa siku makumi ine, muchana na usiku, mpaka Horebu kwenye mulima wa Mungu.


Musa alipoambiwa kwamba baba mukwe wake pamoja na muke wake na wana wake wawili wanakuja,


wakuwe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Yawe nitashuka juu ya mulima Sinai mbele ya watu wote.


Walipoondoka Refidimu na kufika jangwa la Sinai, kule wakapiga kambi mbele ya mulima Sinai.


Yawe akashuka juu ya mulima Sinai, akamwita Musa kutoka kule juu, naye Musa akapanda juu ya mulima.


Basi, Musa akaondoka pamoja na Yoshua, mutumishi wake, akaenda kwenye mulima wa Mungu.


Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.


Mungu akamwambia: “Hakika nitakuwa pamoja nawe. Utawatoa watu wa Israeli na kuja kuniabudu mimi Mungu juu ya mulima huu. Hicho kitakuwa kitambulisho kwamba ni mimi Mungu niliyekutuma wewe.”


Yawe akamwambia Haruni: “Kwenda katika jangwa ukutane na Musa.” Basi, Haruni akaenda, akakutana na Musa kwenye mulima wa Mungu, akamubusu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ