Basi, Musa akatwaa muke wake na watoto wake, akawapandisha juu ya punda, akaanza safari ya kurudi Misri. Katika mukono wake alishika ile fimbo aliyoamuriwa na Mungu aitwae.
Watu hawa wote walikufa katika imani pasipo kupokea mambo Mungu aliyoahidi. Lakini waliyaona kwa mbali na kuyafurahia, wakikubali kwamba walikuwa wageni na wasafiri katika dunia.
Watu wa kabila la Dani wakaisimika ile sanamu ya kuchonga, naye Yonatani mwana wa Gersoni, mujukuu wa Musa, akakuwa kuhani wao. Wazao wake vilevile walikuwa makuhani wa kabila la Dani mpaka wanainchi wa inchi hiyo walipopelekwa katika uhamisho.