Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Kutoka 18:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yetro, kuhani wa Midiani, baba mukwe wa Musa, alisikia juu ya mambo yote ambayo Yawe alimutendea Musa na Waisraeli alipowatoa katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Kutoka 18:1
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi akawaondoa watu wake katika inchi, wachaguliwa wake wakaimba na kushangilia.


Mukumbuke matendo ya ajabu aliyotenda, miujiza yake na hukumu alizotoa,


Ni nani anayeweza kutaja matendo ya Yawe? Ni nani anayeweza kumusifu kama anavyostahili?


Nitamutukuza Yawe nyakati zote, sitaacha hata kidogo kutaja sifa zake.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Mashairi ya Wakora.


Hatutayaficha kwa watoto wetu lakini tutawaelezea kizazi kinachokuja matendo ya utukufu ya Yawe na uwezo wake; tutawaambia maajabu yake aliyotenda.


Basi, wabinti saba wa kuhani mumoja wa kule Midiani wakafika kuchota maji na kuwakunywesha kondoo na mbuzi wa baba yao.


Walipomurudilia baba yao Rueli, yeye akawauliza: “Mbona leo mumerudi upesi hivyo?”


Musa akakubali kukaa kwa yule mutu. Basi, yule mutu akamupa Musa binti yake anayeitwa Zipora akuwe muke wake.


Siku moja, Musa alikuwa anachunga kundi la kondoo la baba mukwe wake Yetro, kuhani wa Midiani. Musa akapeleka kundi lile upande wa magaribi wa jangwa, akafika kwenye mulima Horebu, mulima wa Mungu.


Musa akarudi kwa Yetro, baba mukwe wake, akamwambia: “Tafazali uniruhusu nirudie Misri kwa wandugu zangu, nione kama wangali wazima.” Yetro akamwambia: “Kwenda kwa amani.”


Kwa hiyo, uwaambie Waisraeli hivi: ‘Mimi ni Yawe! Mimi nitawatoa katika nira mulizowekewa na Wamisri. Nitawaokoa toka utumwa wenu. Nitanyoosha mukono wangu wenye nguvu na kuwaazibu vikali Wamisri na kuwakomboa ninyi.


Nao muji huu utakuwa kwangu jina la furaha, sifa na utukufu mbele ya mataifa yote katika dunia ambayo yatasikia juu ya mema yote ninayowafanyia. Mataifa yataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mema na amani nitakazouletea muji huu wa Yerusalema.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Wakati ule, watu kumi kutoka mataifa ya kila luga watamukamatilia Muyuda mumoja na kushika nguo yake na kumwambia: Tunataka kwenda pamoja nanyi, kwa sababu tumesikia kwamba Mungu yuko pamoja nanyi.


Musa akamwambia shemeki yake Hobabu mwana wa Reueli Mumidiani, baba mukwe wake: Sisi tunasafiri kwenda pahali ambapo Yawe amesema: Nitawapa ninyi pahali hapo. Basi, tuende pamoja, nasi tutakutendea vizuri maana Yawe ameahidi kutendea Waisraeli vizuri.


Walipofika Antiokia, wakafanya mukutano wa kanisa na kuwaelezea mambo yote Mungu aliyofanya kwa njia yao, na namna alivyowafungulia watu wa mataifa mengine mulango kusudi wao vilevile wapate kuamini.


Basi mukutano wote ukabaki kimya ukisikiliza maelezo ya Barnaba na Paulo juu ya vitambulisho na maajabu yote Mungu aliyofanya kwa njia yao katikati ya watu wa mataifa mengine.


Kwa maana sitasubutu kuongeza kitu kingine, isipokuwa tu kile Kristo alichotimiza kwa njia yangu kusudi watu wa mataifa wapate kumutii Mungu. Alifanya vile kwa njia ya yale aliyoniwezesha kusema na kutenda,


Maana tumesikia jinsi Yawe alivyoyakausha maji ya bahari Nyekundu mbele yenu mulipotoka inchi ya Misri, na jinsi mulivyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ngambo ya muto Yordani, ni kusema Sihoni na Ogi, ambao muliwaangamiza kabisa.


Wakamujibu: “Sisi, watumishi wako, tumetoka inchi ya mbali na tumekuja kwa maana tumesikia sifa za jina la Yawe, Mungu wenu. Tulipata habari za utukufu wake na yote aliyoyafanya katika inchi ya Misri.


Wazao wa Keni ambaye alikuwa baba mukwe wa Musa, walifuatana na watu wa kabila la Yuda kutokea Muji wa Miti ya Ngazi, ni kusema muji wa Yeriko, mpaka jangwa la Yuda karibu na Aradi, wakafanya makao yao kule pamoja na watu wa Yuda.


Wakati ule, Mukeni mumoja aliyeitwa Heberi alikuwa amejitenga na Wakeni wenzake ambao ni wazao wa Hobabu, baba mukwe wa Musa. Alikuwa amepiga hema lake mbali kule kwenye muti wa mwalo wa Sananimu, karibu na Kedesi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ